Monday, June 1, 2020
Donald TRUMP Muoga Sana... Akimbilia Chumba cha Chini ya ARDHI Baada ya Waandamanaji Kuidhingira IKULU Yote.....
Maandamano ya kupinga kuuawa kwa Mmarekani mweusi, George Floyd yamepelekea Washington DC kutangaza muda wa wananchi kubaki ndani baada ya Maandamano hayo kufanyika karibu na Ikulu (White House)
Kutokana na vurugu zilizokuwa zikiendelea nje ya White House, imeelezwa kuwa Usalama wa Taifa walimpeleka Rais Donald Trump kwenye chumba cha chini cha ardhi (Bunker) ambacho kilitumika wakati wa mashambulio ya kigaidi zamani
Mabomu ya machozi yametumika kuwatawanya waandamanaji zaidi ya 1,000 waliokuwa nje ya Ikulu na mabango huku wakiimba na kuwasha moto. Tangu kuanza kwa maandamano, inadaiwa takriban watu 4,100 wamekamatwa kutokana na makosa ya kuvunja maduka, kufunga barabara na kutozingatia muda wa kutotoka ndani
Mamlaka zimeweka zuio la muda wa kubaki ndani Washington DC pamoja na miji mingine mikubwa ikiwemo Atlanta, Chicago, Denver, Los Angeles, San Francisco na Seattle ili kudhibiti waandamanaji wanaopinga ukatili unaofanywa na Polisi mitaani
George Floyd alifariki dunia Jumatatu iliyopita huko Minneapolis baada ya Polisi mzungu, Derek Chauvin kumkandamiza shingoni kwa kutumia goti. Tangu tukio hilo, Chauvin pamoja na maafisa wengine watatu waliokuwepo wamefukuzwa kazi
Chauvin amefunguliwa mashtaka ya mauaji lakini waandamanaji wameendelea kudai hiyo haitoshi huku wakitaka Polisi wengine watatu waliokuwepo kushtakiwa
Source
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Kupitia ukurasa wake wa Instagram mjasiriamali Faiza Ally ameweka wazi hisia zake na kusema kuwa anatamani sana kuona msanii wa Bongo Flev...
-
UNAPOTAJA jina la mwanamuziki mkubwa barani Afrika, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' kutoka Tanzania, akili za wengi zinakimbilia kwe...
-
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya siku tano ya kunyesha mvua kubwa inayoweza kusababisha athari ikiwemo mafuriko. ...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...