Monday, June 1, 2020
Donald TRUMP Muoga Sana... Akimbilia Chumba cha Chini ya ARDHI Baada ya Waandamanaji Kuidhingira IKULU Yote.....
Maandamano ya kupinga kuuawa kwa Mmarekani mweusi, George Floyd yamepelekea Washington DC kutangaza muda wa wananchi kubaki ndani baada ya Maandamano hayo kufanyika karibu na Ikulu (White House)
Kutokana na vurugu zilizokuwa zikiendelea nje ya White House, imeelezwa kuwa Usalama wa Taifa walimpeleka Rais Donald Trump kwenye chumba cha chini cha ardhi (Bunker) ambacho kilitumika wakati wa mashambulio ya kigaidi zamani
Mabomu ya machozi yametumika kuwatawanya waandamanaji zaidi ya 1,000 waliokuwa nje ya Ikulu na mabango huku wakiimba na kuwasha moto. Tangu kuanza kwa maandamano, inadaiwa takriban watu 4,100 wamekamatwa kutokana na makosa ya kuvunja maduka, kufunga barabara na kutozingatia muda wa kutotoka ndani
Mamlaka zimeweka zuio la muda wa kubaki ndani Washington DC pamoja na miji mingine mikubwa ikiwemo Atlanta, Chicago, Denver, Los Angeles, San Francisco na Seattle ili kudhibiti waandamanaji wanaopinga ukatili unaofanywa na Polisi mitaani
George Floyd alifariki dunia Jumatatu iliyopita huko Minneapolis baada ya Polisi mzungu, Derek Chauvin kumkandamiza shingoni kwa kutumia goti. Tangu tukio hilo, Chauvin pamoja na maafisa wengine watatu waliokuwepo wamefukuzwa kazi
Chauvin amefunguliwa mashtaka ya mauaji lakini waandamanaji wameendelea kudai hiyo haitoshi huku wakitaka Polisi wengine watatu waliokuwepo kushtakiwa
Source
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
