Monday, June 1, 2020

Donald TRUMP Muoga Sana... Akimbilia Chumba cha Chini ya ARDHI Baada ya Waandamanaji Kuidhingira IKULU Yote.....



Maandamano ya kupinga kuuawa kwa Mmarekani mweusi, George Floyd yamepelekea Washington DC kutangaza muda wa wananchi kubaki ndani baada ya Maandamano hayo kufanyika karibu na Ikulu (White House)

Kutokana na vurugu zilizokuwa zikiendelea nje ya White House, imeelezwa kuwa Usalama wa Taifa walimpeleka Rais Donald Trump kwenye chumba cha chini cha ardhi (Bunker) ambacho kilitumika wakati wa mashambulio ya kigaidi zamani

Mabomu ya machozi yametumika kuwatawanya waandamanaji zaidi ya 1,000 waliokuwa nje ya Ikulu na mabango huku wakiimba na kuwasha moto. Tangu kuanza kwa maandamano, inadaiwa takriban watu 4,100 wamekamatwa kutokana na makosa ya kuvunja maduka, kufunga barabara na kutozingatia muda wa kutotoka ndani

Mamlaka zimeweka zuio la muda wa kubaki ndani Washington DC pamoja na miji mingine mikubwa ikiwemo Atlanta, Chicago, Denver, Los Angeles, San Francisco na Seattle ili kudhibiti waandamanaji wanaopinga ukatili unaofanywa na Polisi mitaani

George Floyd alifariki dunia Jumatatu iliyopita huko Minneapolis baada ya Polisi mzungu, Derek Chauvin kumkandamiza shingoni kwa kutumia goti. Tangu tukio hilo, Chauvin pamoja na maafisa wengine watatu waliokuwepo wamefukuzwa kazi

Chauvin amefunguliwa mashtaka ya mauaji lakini waandamanaji wameendelea kudai hiyo haitoshi huku wakitaka Polisi wengine watatu waliokuwepo kushtakiwa
Source
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...