Saturday, May 2, 2020
Spika Ndugai afunguka kuhusu agizo la Mbowe kwa wabunge wa CHADEMA
Spika wa Bunge Job Ndugai, amesema kuwa kauli ya Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe, haimbabaishi na chochote kwa kuwa kila jambo lao wanaweka upinzani na Wabunge ni timu moja na yeye ameamrisha timu yake tu bila kushirikisha wenzake, hivyo Wabunge wa CCM watabaki na kuendeshesha Bunge.
Spika Ndugai ameyabainisha hayo leo Mei 2, 2020, wakati akizungumza , na kuongeza kuwa agizo la Mbowe kwa Wabunge wake wamelipokea kwa mikono miwili, na kwamba amekuwa ni kiongozi wa kuamrisha tu na ndiyo maana wanachama wake wengi wanahama, na kuongeza kuwa janga la Corona ni la Dunia nzima na hakuna ambaye anapenda kuona watu wakifa.
"Sisi halitushangazi hawa wenzetu kila jambo lazima waweke upinzani hata kama ni janga, Wabunge ni timu moja hauwezi kuamrisha tu wachezaji wako kwamba tokeni bila kuzungumza na wenzako, Wabunge wa CHADEMA wana bahati mbaya sana kazi yao ni kuamrishwa tu kama watoto wa Primary vile na wanalalamika kimya kimya sana kwangu" amesema Spika Ndugai.
Aidha Spika Ndugai alizungumzia suala la kupokea ushauri wa Mbowe "Wala siko tayari tena, yeye aendelee tu na Methodology zake kwa sababu muda mfupi ujao tutamaliza Bunge kwa kuzingatia tatizo la Corona na toka tumeanza tumezingatia na tumebadilisha mambo mengi sana".
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
