Mtu mmoja aliyesadikia kuwa ni jangili wa wanyama aina ya faru ameuawa na Tembo kisha kuliwa na Simba katika hifadhi ya taifa ya Kruger, nchini Afrika Kusini.
Kwa mujibu wa mamlaka ya utafiti nchini humo, baada ya uchunguzi imeweza kugundua fuvu pamoja na masalia ya nguo ya mtu huyo.
Pia Mamlaka ya Hifadhi za Taifa nchini iliseme Ijumaa kuwa jangili huyo pamoja na washirika wenzake wanne walikuwa wakijaribu kuwinda wanyama aina ya faru, jioni ya Jumanne, ambapo washirika hao waliiambia familia ya marehemu kuwa mwenzao ameuawa na Tembo.
Mkurugenzi wa hiadhi hiyo ametoa salamu za rambirambi kwa familia huku akitoa angalizo kuwa, ''kuingia kwenye mbuga ya Kruger kinyume cha sheria na kwa miguu si jambo jema,'' alisema Murugenzi huyo. ''ni mbuga yenye hatari nyingi na tukio hili linadhihirisha hayo''.
Hifadhi ya Kruger imekua ikikabiliwa na changamoto ya uwindaji haramu kutokana na uhitaji mkubwa wa pembe za faru kwenye nchi za bara la Asia.
Nchi ya Afrika Kusini ina takribani faru 20,000, ambayo ni asilimia 80 ya faru wote wanaopatikana dunia nzima. Tangu mwaka 2008, jumla ya faru 7,000 wamewindwa kinyume na utaratibu nchini humo, ambapo 1028 kati yao wakiuawa katika mwaka 2017 pekee.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
