Mtu mmoja aliyesadikia kuwa ni jangili wa wanyama aina ya faru ameuawa na Tembo kisha kuliwa na Simba katika hifadhi ya taifa ya Kruger, nchini Afrika Kusini.
Kwa mujibu wa mamlaka ya utafiti nchini humo, baada ya uchunguzi imeweza kugundua fuvu pamoja na masalia ya nguo ya mtu huyo.
Pia Mamlaka ya Hifadhi za Taifa nchini iliseme Ijumaa kuwa jangili huyo pamoja na washirika wenzake wanne walikuwa wakijaribu kuwinda wanyama aina ya faru, jioni ya Jumanne, ambapo washirika hao waliiambia familia ya marehemu kuwa mwenzao ameuawa na Tembo.
Mkurugenzi wa hiadhi hiyo ametoa salamu za rambirambi kwa familia huku akitoa angalizo kuwa, ''kuingia kwenye mbuga ya Kruger kinyume cha sheria na kwa miguu si jambo jema,'' alisema Murugenzi huyo. ''ni mbuga yenye hatari nyingi na tukio hili linadhihirisha hayo''.
Hifadhi ya Kruger imekua ikikabiliwa na changamoto ya uwindaji haramu kutokana na uhitaji mkubwa wa pembe za faru kwenye nchi za bara la Asia.
Nchi ya Afrika Kusini ina takribani faru 20,000, ambayo ni asilimia 80 ya faru wote wanaopatikana dunia nzima. Tangu mwaka 2008, jumla ya faru 7,000 wamewindwa kinyume na utaratibu nchini humo, ambapo 1028 kati yao wakiuawa katika mwaka 2017 pekee.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
