Thursday, October 4, 2018
Mhadhiri UDOM anaswa na Takukuru kisa rushwa ya ngono
Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa mkoa wa Dodoma TAKUKURU, inamshikilia mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) Jacob Nyangusi, kwa kosa la kumtaka kingono mwanafunzi wa mwaka wa kwanza ili amsaidie katika mitihani.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Dodoma Sostenes Kibwengo, Mhadhiri huyo wa Kitivo cha Sayansi ya Jamii katika Chuo Kikuu cha Dodoma ametenda kosa hilo kinyume na kifungu cha 25 cha Sheria ya kuzuia na Kupambana na rushwa Na. 11/2007.
Kibwengo amesema kuwa Mhadhiri huyo alikamatwa saa tatu usiku katika eneo la nyumba mia tatu kata ya Nzuguni jijini Dodoma akiwa chumbani na mwanafunzi huyo.
Amesema Takukuru ilipokea taarifa za Mhadhiri huyo kutaka rushwa ya ngono kwa mwanafunzi wake (jina limehifadhiwa), ili amwezeshe kufanya mitihani ya marudio baada ya kufeli na pia amsaidie wakati wa usahihishaji.
Amesema baada ya kupokea taarifa hizo Takukuru ilifanya uchunguzi wa awali na kuandaa mtego uliofanikisha kukamatwa kwake.
Takukuru inaendelea na uchunguzi na mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani pindi kibali cha Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kikitolewa.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...