Monday, August 6, 2018
Wachezaji wa Simba waikubali Coastal Union
Wachezaji wa Simba waliotolewa kwa mkopo kwenda Coastal Union ya Tanga, Moses Kitandu na Haji Ugando wameeleza kuridhishwa na mwenendo wa mazoezi chini ya kocha Juma Mgunda huku wakiahidi kuwa wapo tayari kujitoa kwaajili ya timu hiyo.
Akiongea baada ya mazoezi ya jana, mshambuliaji Haji Ugando, alisema kuwa Coastal ni timu nzuri na ina mwalimu ambaye anajua ugumu wa ligi hivyo kama mchezaji anafuata maelekezo ya kocha huku yeye binafsi akijiandaa kuhakikisha anacheza mechi zote.
Kwa upande wake Moses Kitandu ambaye msimu uliopita alikuwa mshambuliaji chaguo la pili baada ya John Bocco kwa wekundu wa msimbazi, yeye amekiri kuwa mzunguko wa ligi ni mrefu lakini amejiandaa kushirikiana na wenzake ili kuipa timu hiyo matokeo mazuri.
Kwa upande wake kocha wa timu hiyo Juma Mgunda, ameeleza kuwa kila mchezaji anajituma na kuonesha uwezo kwenye mazoezi. ''Tunafanya mazoezi mara mbili kwa siku na wachezaji wananipa imani kuwa tutashindana kwenye ligi''.
Coastal United ni miongoni mwa timu 6 ambazo zimepanda ligi kuu msimu huu. Timu hiyo ilishuka daraja msimu wa 2016/17, ikacheza ligi daraja la kwanza msimu wa 2017/18 na kufanikiwa kurejea ligi kuu na itaanza msimu wa 2018/19, Agosti 22 kwa kuikaribisha Lipuli FC.
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Siku moja baada ya Israel kusema kuwa inazidisha uvamizi wake wa ardhini nchini Lebanon, Hezbollah inadai iliwafukuza wanajeshi wa Israel ...
-
Kupitia ukurasa wake wa Instagram mjasiriamali Faiza Ally ameweka wazi hisia zake na kusema kuwa anatamani sana kuona msanii wa Bongo Flev...
-
UNAPOTAJA jina la mwanamuziki mkubwa barani Afrika, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' kutoka Tanzania, akili za wengi zinakimbilia kwe...
-
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya siku tano ya kunyesha mvua kubwa inayoweza kusababisha athari ikiwemo mafuriko. ...