Source
Friday, August 13, 2021
WACHAWI WAZUA GUMZO BAADA KUTUPA JENEZA LENYE VITU VYA AJABU MLANGONI
Source
Kumekucha..Sabaya Awataja Magufuli, Dk Mpango na Gavana BoT Kuwa Walifahamu Operesheni Aliyokuwa Akiifanya Arusha.
Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya amewataja Hayati John Magufuli, Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango na Gavana wa Benki Kuu kuwa walikuwa wanajua operesheni aliyokuwa akiifanya Arusha.
Dar es Salaam. Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya leo Ijumaa Agosti 13, 2021 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha amewataja Hayati John Magufuli, Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango na Gavana wa Benki Kuu kuwa walikuwa wanajua operesheni aliyokuwa akiifanya Arusha.
Sabaya amesema hayo wakati akitoa utetezi mbele ya Hakimu mkazi mwandamizi Odira Amworo kuwa alichokuwa anakifanya Arusha Februari 9, 2021 haikuwa operesheni yake ya kwanza kuagizwa na hayati Rais Magufuli
Diwani wa CCM aangua kilio mahakamani akisimulia namna Sabaya alivyomtisha kwa bastol
Akiongozwa na Wakili anayemtetea Mosses Mahuna, wakati alipoanza kujitetea mahakamani hapo amesema kesi hiyo ni ya kutengeneza na yeye hajaiba wala kumtishia mtu yoyote kwa silaha.
Sabaya alisema siku ya tukio Februari 9, 2021 alipomaliza kuongoza kikao cha kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Hai, alipokea simu ya Dk Magufuli aliyemwelekeza kazi ya kufanya katika mkoa wa Arusha ambapo pia alipaswa kuwapitia watu wengine wanne katika uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), ambapo watu hao walikuwa na maelekezo juu ya kazi hiyo wanayoenda kufanya.
"Hiyo haikuwa kazi ya kwanza kwa sababu miezi michache iliyopita tulipewa zoezi la kukamata mitambo inayotengeneza noti bandia na tulifanikiwa kukamata mitambo na fedha Sh 800 Milioni bandia eneo la Chanika wilaya ya Temeke mkoa wa Dar es Salaam ,Gavana wa BoT anajua na aliyekuwa Waziri wa Fedha kwa wakati huo Dk Philip Mpango, Makamu wa Rais wa sasa pia anafahamu,"
IGP Sirro akemea wanaojihusisha na dawa za kulevya
Kina Mbowe waigeuzia kibao Serikali, Hakimu atoa agizo
STEVE NYERERE : MSISIKILIZE WAPOTOSHAJI KUHUSU CHANJO KACHANJENI
Source
Mwenyekiti wa Kampuni za Asas Group, Alhaj Faraj Ahmed Abri Afariki Dunia
Mwenyekiti wa Kampuni za Asas Group, Alhaj Faraj Ahmed Abri amefariki dunia leo Ijumaa Agosti 13 alfajiri, akiwa jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka katika familia hiyo, Mzee Abri atazikwa leo baada ya Swala ya adhuhuri katika makaburi ya Kisutu Dar es Salaam.
"Hakutakuwa na mikusanyiko kwa tutakaokuwa Iringa, tafadhali tutumie zaidi teknolojia za habari kutoa pole na shughuli nyingine," imeeleza taarifa hiyo.
Source
ULEGA ATAKA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI KUKOMESHWA NCHINI
Na. Edward Kondela
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amewataka viongozi wa maeneo mbalimbali nchini kuanzia ngazi ya kijiji kuhakikisha wanasimamia haki na amani na kujiepusha na vitendo vya rushwa ili kudhibiti migogoro ya wakulima na wafugaji.
Naibu Waziri Ulega amebainisha hayo (12.08.2021) wakati alipofanya ziara ya kikazi ya siku moja katika Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga na kuibainisha hayoa kwenye kikao chake na uongozi wa wilaya hiyo na kuwataka pia wataalam wa sekta ya mifugo washirikiane vyema na viongozi katika kutoa pia elimu juu ya umuhimu wa makundi hayo mawili ya wakulima na wafugaji.
Mhe. Ulega amesema wafugaji lazima waishi kwa upendo maeneo walipo pamoja na wafugaji wengine na wakulima kwa kuwa ni dhambi kubwa kuchukua mifugo na kuingiza kwa makusudi kwenye shamba la mkulima.
"Kitendo cha ng'ombe kupelekwa kwenye mashamba ni jinai kama jinai nyingine siyo haki kwa mkulima au mfugaji kuchukua hatua kinyume na taratibu na viongozi wa kijiji wawe wasimamizi wa haki na amani na wasifanye upendeleo pamoja na kufanya vitendo vyovyote vya rushwa." amesema Mhe. Ulega
Naibu Waziri Ulega amelazimika kutoa maelekezo hayo baada ya kupokea taarifa ya uongozi wa Wilaya ya Handeni kuwa kumejitokeza migogoro baina ya wakulima na wafugaji hadi kusababisha vifo vya baadhi ya wakazi wa wilaya hiyo hali ambayo imekuwa ikisababisha hofu ya mahusiano baina ya makundi hayo mawili.
Katika taarifa hiyo wameiomba Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuhakikisha inaweka mikakati mbalimbali ya kukomesha migogoro hiyo ambayo imekuwa ikisababisha hofu, ukizingatia Wilaya ya Handeni ina mifugo mingi na imekuwa ikifanya biashara ya kupeleka mifugo ndani na nje ya nchi.
Chama kujiunga na Klabu ya RS Berkane ya Morocco
CLATOUS Chama kiungo namba moja kwa kutengeneza pasi za mwisho anatajwa kujiunga na Klabu ya RS Berkane ya Morocco kwa dili la miaka mitatu.
Ndani ya Ligi Kuu Bara kwa msimu wa 2020/21 nyota huyo alitengeneza jumla ya pasi 15 na alifunga mabao nane akiwa ni namba moja kwa utengenezaji wa pasi ndani ya ligi.
Taarifa zimeeleza kiungo huyo hatakuwa sehemu ya kikosi cha Simba kwa msimu ujao wa 2021/22.
Mbali na Chama pia nyota wao Luis Miquissone yupo kwenye hesabu za mwisho kutua nchini Misri kwa ajili ya kujiunga na Klabu ya Al Ahly ya Misri.
Tayari jezi namba 11 ambayo aliyokuwa anavaa Luis amekabidhiwa kiungo mpya Peter Banda ambaye anatajwa kuwa mbadala wa nyota huyo.
Simba imeweka kambi nchini Morocco kwa ajili ya maandalizi ya msimu ujao wa 2021/22 ambapo Luis hakuwa sehemu ya kikosi hicho ambacho kipo kambini.
Serikali ya Canada kuanzisha kutoa hati ya chanjo kwa ajili ya safari za kimataifa
Mendicino, ambaye hakutoa tarehe halisi, alisema kuwa mpango huo utatekelezwa katika siku za kwanza za msimu wa vuli.
Akielezea kuwa serikali yake inafanya kazi na nchi zingine kutambua hati za chanjo, Mendicino alisema kuwa watu wa Canada waliopata chanjo kikamilifu wataweza kupata hati ya serikali ambayo itathibitisha historia yao ya chanjo ya Kovid-19 kwa sababu za kusafiri kimataifa.
Mendicino pia alisisitiza kuwa hati ya chanjo itakayotolewa itajumuisha data juu ya aina, tarehe na mahali pa chanjo zilizotolewa, na kubainisha kuwa utumiaji wa hati iliyoandaliwa kwa safari za kimataifa baina ya nchi imeachwa kwa uamuzi wa serikali za majimbo.
Mfumo wa hati ya chanjo, ambao unaendelea kutumika Bulgaria, Jamhuri ya Czech, Denmark, Ujerumani, Ugiriki, Croatia na Poland, pia ulianzishwa huko Japan mnamo Julai.
Wale wanaotumia programu ya ArriveCAN, ambayo Canada ilizindua mnamo Julai, wameondolewa ulazima wa kukaa karantini wanapoingia nchini ikiwa watathibitisha maelezo yao na kujaza data zinazohitajika kwenye programu.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...