Tuesday, October 2, 2018

Mapya yaibuka Birthday ya Diamond, Zari atuma ujumbe wa utata

Leo ni siku ya kuzaliwa kwa muimbaji Diamond Platnumz, watu wake wa karibu, ndugu, marafiki na mashabiki wamekuwa wakimtumia salamu za kheri kwenye siku yake hiyo muhimu.

Ujumbe wa Zari The Bosslady ulikuwa ukisubiriwa sana mara baada ya Diamond kumuandika ujumbe mzuri sana mrembo huyo siku kadhaa zilizopita kwenye Birthday licha ya kuachana kwao.

Sasa Zari The Bosslady ametumia ukurasa wake wa Instagram na kuposti picha ya watoto wake na Diamond kisha kuandika ujumbe wa dharau; 'Happy birthday mwenye vikima vyake'.

Kwa ujumbe huo, watu wengi wamesikitishwa na kitendo cha mwanamama huyo kuwafananisha watoto wa Diamond Platnumz na mnyama KIMA.


Butterfly farmers call upon govt to lift exportation ban

Conservationists who initiated butterfly farming in East Usambara in Tanga Region are still at crossroads following the government's exportation ban.
Source

Diamond aonyesha mjengo wake mpya siku ya birthday yake ( VIDEO)

Msanii wa muziki wa kizazi kipya na C.E.O wa WCB Wasafi Diamond Platnumz ameweza kuonyesha nyumba yake mpya jioni ya leo ikiwa ni siku ake ya kuzaliwa. Msanii alikuwa kwenye show yake nchini Zambia hivyo baada ya kurejea ameweza kutumia akauti yake ya instagram kupitia insta stori kutuonyesha nyumba yake mpya akiwa na wasanii wenzake …

The post Diamond aonyesha mjengo wake mpya siku ya birthday yake ( VIDEO) appeared first on Bongo5.com.


Source

Hii Tabia ya Simu za Mabinti Kuharibika Mnapoanza Uhusiano Imekaaje?


Bandugu,

Imekuwa kama fashion siku hizi ukianza uhusiano na binti, ile mmebadilishana namba na kesho ndo first date, tarajia kuambiwa 'simu imeingia maji, imechukuliwa na mwenyewe' na upuuzi kama huo

Wanafanya hivyo ili akuingize king umtumie hela

Nime experience kwa mabinti kama watatu hasa under 25s! Sasa sijui kwanini hawaambiani kuwa hii trick imegundulika wabadili gia wanajichora sana...

Kevin


Monday, October 1, 2018

Spika Ndugai amuandikia barua Mwenyekiti wa NEC kujiuzulu kwa Mbunge wa Chadema


Kufuatia kujiuzulu ubunge wa Jimbo la Serengeti mkoani Mara, Marwa Ryoba Chacha, Spika wa Bunge, Job Ndugai amemuandikia barua Mwenyekiti wa Tume ye Uchaguzi NEC, Jaji Semistacles Kaijage kumfahamisha kuwa jimbo hilo kwa sasa lipo wazi.

Spika Ndugai ameandika barua hiyo kwa mujibu wa kifungu 37(3) cha sheria ya Taifa ya uchaguzi kinachoelekeza kwamba pale ambapo mbunge amejiuzulu, atafariki au ataacha kazi ya ubunge kwa sababu nyingine yoyote tofauti na zilizoainishwa katika kifungu cha 113 cha sheria hiyo, Spika atamjulisha Mwenyekiti wa NEC na kutangaza kwenye gazeti la Serikali kwamba kiti hicho kiko wazi.

Chacha alitangaza kujiuzulu Ubunge na nafasi zake zote za uongozi ndani ya Chadema huku akitangaza kujiunga na Chama cha Mapinduzi kwa kile alichoeleza kuunga mkono juhudi za Rais John Magufuli katika kuwatumikia wananchi wa Tanzania.




Soma Kisa Hichi Kilichomkuta Huyu Baba Baada ya Simu Kuita Bahati Mbaya Akiwa Kanisani


Simu yake iliita kwa Bahati mbaya wakati wa ibada akiwa kanisani 📞☎

Mchungaji alimfokea

Waumini walimzonga baada ya maombi ya ibada
Wakati anarudi nyumbani, njia nzima mkewe aliendelea kumsema kwa kutokuwa makini
Akajisikia vibaya sana, huzuni, na aibu juu

Jioni yake, ili kupoteza mawazo, alikwenda bar

Aliagiza bia, akaiweka mezani. Kwa kuwa alikuwa na mawazo mengi, akaigusa pombe ikamwagika 🍻🍺

Muhudumu alikuja, akampa pole kwa unyenyekevu, na akafuta meza kiustaarabu, kisha akamfuta jamaa ilipommwagikia kiunyenyekevu

Meneja wa bar ile alimpa jamaa bia ya ofa kufidia iliyomwagika 🥂🥃🍾
Muhudumu wa kaunta alipomletea alim'busu akim'bembeleza, "Usijali, hakuna ambaye hana makosa!"

Jamaa hajawahi kukosa 'ibada' ktk bar hiyo tangu siku ile

SOMO:
Unavyowatendea watu kunaweza kujenga au kuwabomoa, hasa wanapokosea.

VIDEO: Kisa Polisi Hashim Rungwe agoma kushiriki uchaguzi ''Hatuwezi kushiriki chaguzi za ugomvi"


Mwanyekiti wa Chama Cha Ukombozi wa Umma (CHAUMA) Hashim Rungwe amefunguka kuhusiana na chama chake kutoonekana kikishiriki chaguzi ndogo zinazoendelea nchini na kubainisha kuwa hawawezi kushiriki chaguzi hizo zilizojaa ugomvi.

''Utafanyaje uchaguzi ambao na polisi wanacheza mchezo huohuo, polisi hatakiwi kwenye uchaguzi sisi tunataka uchaguzi wa haki na kama wasipotaka basi sisi tukakaa kimya tu:" Hashimu Rungwe

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI......USISAHAU KUSUBSCRIBE

Kabla ya kuivaa Valencia Champions League, Mourinho asisitiza wapo wachezaji wanaompa ushirikiano

Meneja wa klabu ya Manchester United, Jose  Mourinho licha ya kuripotiwa kutokuwa na maelewano mazuri na wachezaji wake amesema kuwa wapo ambao anaoelewana nao na kujitolea zaidi. Maneno ya Mourinho yanakuja wakati akitarajia kushuka uwanjani hapo kesho siku ya Jumanne kukabiliana na Valencia mchezo wa klabu bingwa barani Ulaya. Mreno huyo amekuwa kwenye kipindi kigumu …

The post Kabla ya kuivaa Valencia Champions League, Mourinho asisitiza wapo wachezaji wanaompa ushirikiano appeared first on Bongo5.com.


Source

Home affairs minister’s directive on bail applications

Minister of home affairs has directed the police to grant bail to the suspects 24 hours a day provided that they fulfill the requirements.
Source
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...