Sunday, March 14, 2021
Marufuku Wafungwa kutumika kwa kazi binafsi
Serikali imepiga marufuku wafungwa kutoka Magereza mbalimbali nchini kutumika katika kazi binafsi isipokuwa kwa kufuata utaratibu unaotambulika kisheria.
Marufuku hiyo imetolewa leo na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Khamis Hamza Chilo wakati wa kikao kilichojumuisha askari polisi kutoka Idara zilizopo chini ya wizara ikiwepo Jeshi la Polisi,Jeshi la Zimamoto na Uokoaji,Jeshi la Magereza,Uhamiaji na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa,kilichofanyika mkoani Singida.
Naibu Waziri Chilo amesema wafungwa wana taratibu zao zinazowaongoza katika mfumo wao mzima wakiwa gerezani huku akiwaagiza wakuu wa magereza yote nchini kufuata taratibu hizo kwani kutofuata taratibu hizo kutapelekea baadhi ya sheria kuvunjwa.
"Kuna taarifa za uhakika kwa wafungwa kutumika katika shughuli binafsi ikiwemo kujenga nyumba za watu binafsi na kulima mashamba ya watu binafsi,nimpongeze Kamishna Jenerali wa Magereza,Suleiman Mzee katika kipindi chake ameanza kuchukua hatua Madhubuti kuhakikisha jeshi linarudi katika misingi yake na sasa tunaona magereza inaendelea kuboreka kila uchwao,sisi kama serikali tunapiga marufuku matumizi binafsi ya wafungwa katika shughuli yoyote binafsi ila kwa kufuata utaratibu" alisema Naibu Waziri Khamis Hamza Chilo
Katika kikao hicho Naibu Waziri Chilo ameyatoa maelekezo mbalimbali ikiwemo tuhuma za rushwa kwa askari wa usalama barabarani, upelelezi wa kesi kuchukua muda mrefu,changamoto ya Vitambulisho vya Taifa na askari wa Jeshi la Zimamoto kuwahi katika matukio ya uokozi.
"Pamoja na kazi nzuri mnayofanya lazima tukae chini kwa Pamoja tujitathmini ili tuweze kuona namna ya kuwasaidia Watanzania,niagize ni marufuku kwa askari yoyote kuchukua rushwa,tunamalizana na madereva barabarani hatuendani nao kwa mujibu wa taratibu na sheria,wengine tunawabambikizia tu kesi makusudi ili waonekane tu wamefanya makosa,kama tumemuona amefanya kosa mpelekeni kunakohusika pia suala la kuwalimbikiza mahabusu katika vituo vya polisi kwa dhana ya kusubiri upelelezi ambao unachukua muda mrefu sio suala nzuri,nawaomba wapelelezi mfanye kazi yenu,ni marufuku kuwarundika mahabusu ndio maana dhamana ikawepo wapeni dhamana kwa kufuata sheria na taratibu" alisema Naibu Waziri Chilo
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
