Tuesday, June 2, 2020
TCCIA Manyara watoa ushauri TRA kufuatia Malalamiko ya wafanyabiashara
Na John Walter,Manyara
Baadhi ya wafanyabiashara mjini Babati mkoa wa Manyara wakitoa maoni yao juu ya utendaji wa mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) mkoani hapo,wameonyesha kutoridhishwa na namna wanavyohudumiwa.
Wakizungumza na kituo hiki bila kutaja majin yao, wamesema kuwa baadhi ya watumishi katika mamlaka hiyo wamekuwa na tabia ya kukadiria mapato makubwa kwa wafanyabiashara ili kutengeneza meza ya mazungumzo, hatua inayopelekea kutengeneza mazingira ya Rushwa.
Wameipongeza TAKUKURU mkoa wa Manyara kwa kuanza kufuatilia utendaji wa Mamlaka ya Mapato (TRA) huku wakiomba viongozi wa ngazi mbalimbali za serikali, kuwa na utaratibu wa kusikiliza kero zinazowakabili wafanyabiashara.
Katibu wa chama cha wafanyabiashara,wakulima na wenye viwanda (TCCIA) Mkoa wa Manyara Mwanahamisi Hussein amesema ni muda mrefu wafanyabiashara wamekuwa wakiilalamikia mamlaka hiyo.
Katibu huyo ameiomba mamlaka hiyo kuwa na tabia ya kuwatembea wafanyabiashara mara kwa mara na kufuatilia mienendo ya watendaji wao wanaowatuma akieleza kuwa hatua hiyo itasaidia kupunguza kero za muda mrefu za kodi ambazo zimekuwa kikwazo katika ukuaji wa shughuli za biashara nchini.
Katika hatua nyingine Mwanahamisi ameeleza kuwa wameandaa utaratibu maalum wa kusikiliza kero mbalimbali za wafanyabiashara mkoani hapo na kuwapatia ushauri,ambapo huwashirikisha pia Mamlaka ya Mapato Manyara.
Kwa madai ya kusumbuliwa na Mamlaka hiyo taarifa zinaeleza kuwa imepelekea wengine kupata shinikizo la damu huku baadhi wakifunga biashara zao.
Mkuu wa Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa mkoa wa Manyara (TAKUKURU) Holle Mkungu, mwezi Mei,2020 waliwafikisha katika Mahakama ya hakimu mkazi Manyara maafisa wawili wa TRA kwa makosa ya kudai na kupokea Rushwa ya shilingi Milioni kumi.
Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Subilaga Mwangama na Ojungu Mollel, na kwamba walifanya makosa hayo kinyume cha kifungu cha 15 cha sheria ya kuzuia na kupambana na Rushwa namba 11/2007.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango akizungumza bungeni Juni 13, 2019 wakati akiwasilisha bajeti ya Serikali Kuu kwa mwaka 2019/2020, alisema ili kupunguza malalamiko ya wafanyabiashara, Serikali imeamua kuanzisha kitengo huru cha kupokea malalamiko ya taarifa za kodi dhidi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na kusimamiwa na kuratibiwa na wizara yake ili kuhakikisha kinakuwa na ufanisi wa kushughulikia kero za wafanyabiashara.
Alisema majukumu ya kitengo hicho ni kupokea malalamiko ya rushwa dhidi ya watumishi wa TRA ambao wamekuwa wakijipatia fedha kinyume na sheria na kuwakandamiza wafanyabiashara.
Aidha, kitengo hicho kinahusika kupokea malalamiko ya ukadiriaji wa kodi na uthaminishaji wa bidhaa husika pasipo kufuata taratibu zilizowekwa na malalamiko ya matumizi ya nguvu katika ukusanyaji wa kodi dhidi ya TRA.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...