Wednesday, June 3, 2020
Mkoa wa Ruvuma una ziada ya chakula tani 900,000
Na Muhadh Mohammed. Songea Ruvuma.
MKOA wa Ruvuma hadi kufikia Mei mwaka huu una ziada ya chakula zaidi ya tani 900,000.
Hayo amesema na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme wakati anafungua kikao maaluma cha Baraza la madiwani cha kujadili ripoti ya CAG Halmashauri ya Mbinga,kilichofanyika ukumbi wa Benjamini Mkapa katika shule ya sekondari Kigonsera .
Kwa mujibu wa Mkuu wa Mkoa hadi kufikia Mei 15 mwaka huu Mkoa ulikuwa umevuna zaidi ya tani milioni 1.4 za mazao ya chakula na biashara.
''Tunamshukuru Mungu ametupa Mvua nzuri na ametuepusha na wadudu wa haribifu hivyo tunatarajia kuvuna mazao mengi mwaka huu katika Mkoa wetu''.
Hata hivyo Mndeme ametoa raia kwa wakulima wajiepushe kuuza mahindi kwa bei ndogo kwa sababu mahitaji ya chakula mwaka huu ni Makubwa na kwamba walanguzi wananunua kwa bei ndogo hivyo wasifanye haraka kuuza.
Ametoa rai kwa wakulima kusubiri serikali itoe bei nzuri ili wananchi waweze kupata faida badala ya kunyonywa na walanguzi ambao hivi sasa wapo wengi wanapita kwa wakulima ili kununua mazao kwa bei ndogo.
Source
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...