Wednesday, June 3, 2020
Mkoa wa Ruvuma una ziada ya chakula tani 900,000
Na Muhadh Mohammed. Songea Ruvuma.
MKOA wa Ruvuma hadi kufikia Mei mwaka huu una ziada ya chakula zaidi ya tani 900,000.
Hayo amesema na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme wakati anafungua kikao maaluma cha Baraza la madiwani cha kujadili ripoti ya CAG Halmashauri ya Mbinga,kilichofanyika ukumbi wa Benjamini Mkapa katika shule ya sekondari Kigonsera .
Kwa mujibu wa Mkuu wa Mkoa hadi kufikia Mei 15 mwaka huu Mkoa ulikuwa umevuna zaidi ya tani milioni 1.4 za mazao ya chakula na biashara.
''Tunamshukuru Mungu ametupa Mvua nzuri na ametuepusha na wadudu wa haribifu hivyo tunatarajia kuvuna mazao mengi mwaka huu katika Mkoa wetu''.
Hata hivyo Mndeme ametoa raia kwa wakulima wajiepushe kuuza mahindi kwa bei ndogo kwa sababu mahitaji ya chakula mwaka huu ni Makubwa na kwamba walanguzi wananunua kwa bei ndogo hivyo wasifanye haraka kuuza.
Ametoa rai kwa wakulima kusubiri serikali itoe bei nzuri ili wananchi waweze kupata faida badala ya kunyonywa na walanguzi ambao hivi sasa wapo wengi wanapita kwa wakulima ili kununua mazao kwa bei ndogo.
Source
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...