Wednesday, June 3, 2020
Mkoa wa Ruvuma una ziada ya chakula tani 900,000
Na Muhadh Mohammed. Songea Ruvuma.
MKOA wa Ruvuma hadi kufikia Mei mwaka huu una ziada ya chakula zaidi ya tani 900,000.
Hayo amesema na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme wakati anafungua kikao maaluma cha Baraza la madiwani cha kujadili ripoti ya CAG Halmashauri ya Mbinga,kilichofanyika ukumbi wa Benjamini Mkapa katika shule ya sekondari Kigonsera .
Kwa mujibu wa Mkuu wa Mkoa hadi kufikia Mei 15 mwaka huu Mkoa ulikuwa umevuna zaidi ya tani milioni 1.4 za mazao ya chakula na biashara.
''Tunamshukuru Mungu ametupa Mvua nzuri na ametuepusha na wadudu wa haribifu hivyo tunatarajia kuvuna mazao mengi mwaka huu katika Mkoa wetu''.
Hata hivyo Mndeme ametoa raia kwa wakulima wajiepushe kuuza mahindi kwa bei ndogo kwa sababu mahitaji ya chakula mwaka huu ni Makubwa na kwamba walanguzi wananunua kwa bei ndogo hivyo wasifanye haraka kuuza.
Ametoa rai kwa wakulima kusubiri serikali itoe bei nzuri ili wananchi waweze kupata faida badala ya kunyonywa na walanguzi ambao hivi sasa wapo wengi wanapita kwa wakulima ili kununua mazao kwa bei ndogo.
Source
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...