Tuesday, June 2, 2020

Mbunge Monko wa Singida akabidhi vifaa vyenye thamani ya milioni 14

Mbunge wa jimbo la Singida kaskazi Mh Eng Justin Joseph Monko amekabidhi vifaa vyenye thamani ya sh milioni 14 kwa Kata za Ilongero, Merya na Maghojoa ikiwa ni  baadhi ya ahadi zake alizoahidi katika Kata hizo.


Vifaa alivyokabidhi ni pamoja na Bati 100 kwaajili ya ujenzi wa Ofisi ya CCM wilaya ya Singida Vijijini,Mifuko 80 ya Saruji ujenzi wa Kanisa Katolik Ilongero, Mifuko 30 ya Saruji kwajili wa ujenzi wa darasa  shule shikizi ya Mvae Kata ya Merya ,Mifuko 30 kuchangia ujenzi wa nyumbani ya katibu UVCCM wilaya ya Singida Vijijini, Mifuko ya Saruji 10 ujenzi wa nyumbani ya katibu Uvccm Mkoa wa Singida.


Pia amechangia boksi 20 za vitabu ikiwa 16 kwa ni kwaajili ya shule za Sekondari  ambavyo ni vya Sayansi na Sanaa na Boksi 4 kwaajili ya shule za msingi pia Mh Monko amekabidhi bati 40 kwaajili ya ujenzi wa Shule ya msingi Maghojoa.
Source
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...