Wednesday, May 6, 2020
Wakimbizi nusu milioni Kenya hatarini kuambukizwa COVID-19
Karibu wakimbizi nusu milioni wanaoishi katika kambi za wakimbizi Kenya wanakabiliwa na hatari ya kuambukizwa ugonjwa wa COVID-19.
Kwa mujibu wa taarifa wakimbizi hao wanaaishi katika kambi zenye msongamano mkubwa wa watu na suhula duni za kiafya ya kijamii.
Hadi sasa hakuna kesi ya corona iliyoripotiwa katika kambi hizo lakini Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) limetangaza kuna mipango ya kukabiliana na COVID-19.
UNHCR imetahadharisa kuwa, maafa makubwa yataibuka iwapo ugongwa wa COVID-19 utaenea miongoni mwa wakimbizi.
Kambi ya Dadaab iliyoko kaskazini mashariki mwa Kenya ina wakimbizi 211,365 waliosajiliwa na hivyo kuifanya kuwa kambi ya tatu kwa ukubwa duniani. Kambi nyingine kubwa ya wakimbizi nchini Kenya ni ile ya Kakuma iliyo kaskazini mwa nchi hiyo na inakadiriwa kuwa na wakimbizi 194,000. Aghalabu ya wakimbizi nchini Kenya ni kutoka nchi jirani za Somalia na Sudan Kusini.
Hadi sasa watu 535 wameambukizwa COVID-19 na miongoni mwao 182 wamepona na wengine 24 wameaga dunia.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...

