Na Alphonce Kusaga
Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Gabriel Daqqaro amehoji ni kwanini zahanati ya Baraa ujenzi wake ulisimama zaidi ya miaka 12 ilhali hadi sasa halmashauri ya Jiji la Arusha imetoa zaidi ya sh, milioni 84.120
Daqqaro amesema hayo katika Kata ya Baraa wakati wa ziara yake ya kutembelea miradi ya elimu, Afya na Miradi ya Kimkakati (TSCP) iliyoambatana na wataalam wa Jiji la Arusha.
Daqaro amehoji katika kipindi cha miaka 12 wananchi wa kata ya Baraa wanakosa huduma za Afya na kulazimika kupata huduma hizo kata ngingine.
"Nataka kujua ni kwanini ujenzi umechukua muda mrefu huku wananchi wakishindwa kupata huduma za afya katika eneo la karibu na makazi yao"
Kwa upande wa Injinia Samuel Mshuza amesema awali kulikuwa na vipaumbele vingine vilivyopelekea zahanati hiyo kutokamilika kwa wakati pia ramani ya jengo hilo ilibadilishwa lakini sasa wapo katika hatua za mwisho za ujenzi wa zahanati hiyo
Naye Mtendaji wa Kata hiyo ya Baraa, Anna Lebisa alisema kuwa ujenzi wa zahanati hiyo ulianza kutekelezwa mwaka 2008na kusimama kwa zaidi ya miaka 12 lakini hivi sasa wanaishukuru serikali kwa kutekeleza ujenzi huo kwa zaidi ya asilimia 86 ambapo amesema eneo hilo kunachangamoto ya udongo sambamba na maji kutuama
Hata hivyo Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Dk, Maulid Madeni alisema kuwa fedha za ujenzi wa zahanati hiyo zipo na kuwataka wakandarasi wa zahanati hiyo ya Baraa na Hospitali ya Wilaya ya Arusha kusema wanahitaji kiasi gani cha fedha ili waweze kulipwa na ujenzi uendelee
"Namshukuru Rais John Magufuli kwa kutoa fedha kwaajili ya ujenzi wa hospitali na vituo vya afya Mkoa wa Arusha ili kupunguza msongamano wa wagonjwa katika hospitali ya Mkoa ya Mount Meru iliyopo Jijini Arusha" Alisema DC Daqaro
Pia Amesisitiza jengo la wadi ya kinamama na mtoto katika hospitali ya wilaya kumalizika mapema ili kuondoa msongamano katika hospitali ngingine
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
