Na Alphonce Kusaga
Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Gabriel Daqqaro amehoji ni kwanini zahanati ya Baraa ujenzi wake ulisimama zaidi ya miaka 12 ilhali hadi sasa halmashauri ya Jiji la Arusha imetoa zaidi ya sh, milioni 84.120
Daqqaro amesema hayo katika Kata ya Baraa wakati wa ziara yake ya kutembelea miradi ya elimu, Afya na Miradi ya Kimkakati (TSCP) iliyoambatana na wataalam wa Jiji la Arusha.
Daqaro amehoji katika kipindi cha miaka 12 wananchi wa kata ya Baraa wanakosa huduma za Afya na kulazimika kupata huduma hizo kata ngingine.
"Nataka kujua ni kwanini ujenzi umechukua muda mrefu huku wananchi wakishindwa kupata huduma za afya katika eneo la karibu na makazi yao"
Kwa upande wa Injinia Samuel Mshuza amesema awali kulikuwa na vipaumbele vingine vilivyopelekea zahanati hiyo kutokamilika kwa wakati pia ramani ya jengo hilo ilibadilishwa lakini sasa wapo katika hatua za mwisho za ujenzi wa zahanati hiyo
Naye Mtendaji wa Kata hiyo ya Baraa, Anna Lebisa alisema kuwa ujenzi wa zahanati hiyo ulianza kutekelezwa mwaka 2008na kusimama kwa zaidi ya miaka 12 lakini hivi sasa wanaishukuru serikali kwa kutekeleza ujenzi huo kwa zaidi ya asilimia 86 ambapo amesema eneo hilo kunachangamoto ya udongo sambamba na maji kutuama
Hata hivyo Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Dk, Maulid Madeni alisema kuwa fedha za ujenzi wa zahanati hiyo zipo na kuwataka wakandarasi wa zahanati hiyo ya Baraa na Hospitali ya Wilaya ya Arusha kusema wanahitaji kiasi gani cha fedha ili waweze kulipwa na ujenzi uendelee
"Namshukuru Rais John Magufuli kwa kutoa fedha kwaajili ya ujenzi wa hospitali na vituo vya afya Mkoa wa Arusha ili kupunguza msongamano wa wagonjwa katika hospitali ya Mkoa ya Mount Meru iliyopo Jijini Arusha" Alisema DC Daqaro
Pia Amesisitiza jengo la wadi ya kinamama na mtoto katika hospitali ya wilaya kumalizika mapema ili kuondoa msongamano katika hospitali ngingine
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam, imetupilia mbali shauri lililokuwa limefunguliwa na Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina...
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...