Friday, March 27, 2020
Bosi wa TAKUKURU Kinondoni, wenzake wanne wakalia kuti kavu
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) nchini Tanzania imesema itawakamata watumishi wake watano akiwamo mkuu wa taasisi hiyo Mkoa wa Kinondoni jijini Dar es Salaam, Teddy Mjangira ili kujibu tuhuma zinazowakabili.
Akizungumza na Mwananchi leo Alhamisi Machi 26, 2020 kwa simu, Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Brigedia Jenerali John Mbungo amesema watumishi hao kwa pamoja wanatuhumiwa kumfanyia uchunguzi mtumishi wa umma ambaye hakuwa na kosa.
Amesema hatua hiyo ilimsababishia usumbufu usiokuwa wa lazima.
"Tutawakamata, tutawaweka ndani na tutafanya uchunguzi kujua hasa nini kilitokea. Lakini niseme tu kuwa utumishi wa umma unahitaji kuwa na maadili na nidhamu na tuna imani mkuu wetu (wa Kinondoni) amepotoka," amesema Mbungo
Mapema leo Alhamisi asubuhi, Rais wa Tanzania, John Magufuli wakati akipokea taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya mwaka 2018/19 na ya Takukuru ya mwaka 2018/19 Ikulu ya Chamwino, Dodoma aliipongeza taasisi hiyo ya ukaguzi huku akigusia watumishi hao wa Kinondoni bila kufafanua zaidi.
Kutokana na utendaji mzuri wa Takukuru, Rais Magufuli amemdhibitisha Brigedia Jenerali John Mbungo kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru.
Awali, Mbungo alikuwa akikaimu nafasi hiyo yangu Septemba 12, 2019 baada ya aliyekuwa mkurugenzi mkuu, Diwani Athuman kuteuliwa na Rais Magufuli kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa (TISS).
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
