Waziri wa maswala ya kigeni nchini Afrika Kusini ameitisha mkutano wa dharura na mabalozi kufuatia mashambulizi dhidi ya wageni mjini Durban.
Mapema Jumatatu watu watatu walifariki kufuatia maandamano yanayolenga maduka, mengi ambayo yanamilikiwa na wageni.
Takriban watu 50 walitafuta hifadhi katika kituo kimoja cha polisi wakati kundi moja la vijana wa Afrika wasio na kazi walipowashinikiza kutoka katika majumba yao usiku.
Takriban watu 100 walishambulia maduka ya vyakula siku ya Jumapili usiku na Jumatauj alfajiri , wakiiba na kuchoma majumba.
Mwanamke mmoja alifariki wakati alipoanguka kutoka kwa paa la nyumba wakati alipokuwa akiwatoroka waandamanaji hao.
Watu wengine wawili waliuawa kutokana na majeraha ya risasi , baada ya mwenye duka moja kudaiwa kuwapiga risasi.
Siku ya Jumanne wageni walianza kutafuta hifadhi katika misikiti na kituo cha polisi.
Waziri wa mahusiano ya kigeni na ushirikiano Lindiwe Sisulu aliwaagiza maafisa wa polisi kuwakabili watu wanaowashambulia wageni.
''Vitendo vyovyote vya kihuni pamoja na wizi wa mali ya raia wa kigeni hautakubalika na maafisa wa polisi na taasisi za kiusalama zinafaa kuchukua hatua za dharura bila kupendelea upande wowote'', alisema katika taarifa.
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Ameandaa mkutano na wanadiplomasia wa Afrika.
Baadhi ya watu hulalamika kuhusu wageni wanaofanya kazi nchini Afrika Kusini ambapo ukosefu wa ajira uko juu ukiwa asilimia 72 mwisho wa mwaka uliopita.
Mashambulizi dhidi ya wahamiaji kutoka mataifa mengine ya Afrika sio jambo geni nchini Afrika kusini.
Mwaka 2015, ghasia katika miji ya Johannesburg na Durban zilisababisha mauaji ya watu saba baada ya wahamiaji kuwindwa na kushambuliawa na magenge.
Afrika kusini ilikumbwa na ghasia mbaya zaidi dhidi ya wageni mwaka 2008 wakati ambapo zaidi ya watu 60 waliuawa.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
