Afisa Habari wa Simba SC, Haji Manara ameendelea na majigambo yake hasa kwa watani wake Yanga, ambapo amesema kuwa endapo watani zake wa jadi Yanga katika mchezo wake na Tukuyu Stars leo, wakifikisha nusu ya mashabiki waliohudhuria kwenye mchezo wao dhidi ya Nkana FC, yuko yatari kujiuzulua nafasie ya usemaji, ndani ya klabu.
Manara amefunguka hayo kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo ameandika kuwa Simba haiwezi kufananishwa na timu zingine Tanzania wakiwemo watani wake, Yanga.
"Yanga leo wanacheza na Tukuyu Stars, wakijaza asilimia kumi kama jana najiuzulu usemaji wa Simba, halafu yupo mswahili anaweza kuthubutu kunifananisha De la boss na wasemaji wengine?", ameandika Manara.
Yanga inacheza na Tukuyu stars katika dimba la taifa, jijini Dar es salaam katika michuano ya shirikisho (AFC), huku watani wao Simba wakiwa wamefanikiwa kutinga hatua ya makundi ya Klabu Bingwa Afrika kwa mara ya kwanza baada ya miaka 15, wakiichapa Nkana FC ya Zambia.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
