Kama unataka kusonga mbele na kuwa na mafanikio makubwa zaidi, mshirika wa kwanza ambaye unatakiwa kushirikiana naye bila kumwacha hadi akakupa mafanikio hayo ni muda wako ulionao.
Ufanye muda uwe rafiki yako wa karibu sana ili ukupatie mafanikio. Usipoteze muda wako kwa mambo ya hovyo, fanya vitu vyako kwa umakini na mpangilio mkubwa, kila unapotumia muda wako.
Inawezekana maisha yako umekuwa ukiyaona hayafai hasa kwa kuona hujatimiza karibu kila kitu. Hiyo inaweza ikawa ni sawa, lakini wakati na nafasi ya kubadili mambo hayo na kuwa mazuri unayo tena.
Muda ukiutumia vizuri unaweza kukupa uwezo wa kukamilisha mambo ambayo kwa kawaida yalionekana ni magumu kuweza kuyatimiza. Kipi unachokitaka ambacho kitashindikana kwa sababu ya muda.
Je, unataka kuandika kitabu? andika mistari michache kila siku, muda utafika kitabu chako kitakamilika. Je, unataka kujenga biashara yako? anza na biashara yoyote hata kama ni ndogo sana na ikuze kidogo kidogo, muda ukifika itakuwa kubwa sana.
Chochote unachotaka kukifanikisha kwako inawezekana, hata iwe unataka kuongea lugha mpya? jifunze maneno machache kila siku na wakati utafika utafanya kwa ufasaha na kujikuta mzungumzaji tayari.
Kama nilivyotangulia kusema, karibu kitu chochote unachokitaka, kipo ndani ya uwezo wako na unayo nafasi kubwa ya kukifikia ikiwa utaamua kutenga muda wako kufanya jambo hilo na kulifanikisha.
Rafiki wa karibu yako, rafiki ambaye anaweza kukupa mafanikio makubwa sana ni muda wako. Unatakiwa ukae chini na kujiuliza maswali ya msingi, je muda wako unautumia vizuri au hovyo hovyo.
Kama unatumia muda wako hovyo, utakuwa kwenye wakati mgumu sana wa kuweza kubadili hali ya maisha yako na hadi kuwa nzuri. Kumbuka hata ukiwa na hali mbaya vipi, lakini ukiweka juhudi na kujipa muda utafanikiwa.
Hakuna ambaye ameachwa mtupu, kama matumizi ya muda wake ni sahihi. Kama ulikuwa hujaanza kutunza muda wako kwa ajili ya mafanikio, anza leo. Fanya mambo ya kukua mafanikio hata kama ni madogo sana, baada ya miaka michache utafanikiwa.
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Na Amiri Kilagalila Njombe Jumuiya ya wanawake wa Chama cha Mapinduzi CCM mkoa wa Njombe inatarajia kufungua kiwanda cha kuzalisha sabuni mk...
-
UNAPOTAJA jina la mwanamuziki mkubwa barani Afrika, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' kutoka Tanzania, akili za wengi zinakimbilia kwe...
-
Kupitia ukurasa wake wa Instagram mjasiriamali Faiza Ally ameweka wazi hisia zake na kusema kuwa anatamani sana kuona msanii wa Bongo Flev...
-
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya siku tano ya kunyesha mvua kubwa inayoweza kusababisha athari ikiwemo mafuriko. ...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...