Monday, March 22, 2021
Mnangagwa: Msaada wa Magufuli hautasahaulika Zimbabwe
Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe amesema leo ni siku kubwa sana kwa Taifa la Tanzania, lakini pia ni siku kubwa kwa Zimbabwe kwani wananchi wake wanaomboleza na Watanzania kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli.
Akizungumza katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma wakati wa shughuli ya kitaifa ya kuaga mwili wa Dkt Magufuli, Rais Mnangagwa ametoa pole kwa Rais Samia Suluhu Hassan na mke wa Dkt. Magufuli Mama Janeth Magufuli, kwa kumpoteza kiongozi huyo ambaye ni ndugu wa Waafrika na wananchi wote wa Zimbabwe.
Amesema Wananchi wa Zimbabwe wanaendelea kuwaombea Watanzania katika kipindi hiki kigumu.
Rais Mnangagwa amesema Dkt. Magufuli atakumbukwa kuwa ni Mwanaume wa vitendo, aliyesaidia kulijengea heshima Taifa lake, kwani ameharakisha maendeleo ya Taifa hilo.
Rais huyo wa Zimbabwe amesema maendelea ya kiuchumi nchini Tanzania yaliyopatikana chini ya uongozi wa Dkt. Magufuli yalihamasisha wananchi wa Zimbabwe kuamini kuwa nao wanaweza kujipatia maendeleo bila kutegemea misaada kutoka nje.
Amesema Dkt. Magufuli atakumbukwa kwa jinsi alivyosimama kidete kuhakikisha kuwa vikwazo vya kimataifa ilivyowekewa Zimbabwe vinaondolewa.
Aidha amesema Dkt. Magufuli alikuwa kiongozi wa kwanza kuipatia msaada wa chakula nchi yake baada ya kukumbwa na kimbunga Idai, kimbunga kikali kilicholeta maafa makubwa Zimbabwe.
Rais Mnangagwa amesema Zimbabwe itaendelea kumsaidia Rais Samia Suluhu Hassan na Watanzania wote kutimiza ndoto zilizoanzishwa na Dkt. Magufuli.
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
