Monday, March 22, 2021
Mnangagwa: Msaada wa Magufuli hautasahaulika Zimbabwe
Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe amesema leo ni siku kubwa sana kwa Taifa la Tanzania, lakini pia ni siku kubwa kwa Zimbabwe kwani wananchi wake wanaomboleza na Watanzania kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli.
Akizungumza katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma wakati wa shughuli ya kitaifa ya kuaga mwili wa Dkt Magufuli, Rais Mnangagwa ametoa pole kwa Rais Samia Suluhu Hassan na mke wa Dkt. Magufuli Mama Janeth Magufuli, kwa kumpoteza kiongozi huyo ambaye ni ndugu wa Waafrika na wananchi wote wa Zimbabwe.
Amesema Wananchi wa Zimbabwe wanaendelea kuwaombea Watanzania katika kipindi hiki kigumu.
Rais Mnangagwa amesema Dkt. Magufuli atakumbukwa kuwa ni Mwanaume wa vitendo, aliyesaidia kulijengea heshima Taifa lake, kwani ameharakisha maendeleo ya Taifa hilo.
Rais huyo wa Zimbabwe amesema maendelea ya kiuchumi nchini Tanzania yaliyopatikana chini ya uongozi wa Dkt. Magufuli yalihamasisha wananchi wa Zimbabwe kuamini kuwa nao wanaweza kujipatia maendeleo bila kutegemea misaada kutoka nje.
Amesema Dkt. Magufuli atakumbukwa kwa jinsi alivyosimama kidete kuhakikisha kuwa vikwazo vya kimataifa ilivyowekewa Zimbabwe vinaondolewa.
Aidha amesema Dkt. Magufuli alikuwa kiongozi wa kwanza kuipatia msaada wa chakula nchi yake baada ya kukumbwa na kimbunga Idai, kimbunga kikali kilicholeta maafa makubwa Zimbabwe.
Rais Mnangagwa amesema Zimbabwe itaendelea kumsaidia Rais Samia Suluhu Hassan na Watanzania wote kutimiza ndoto zilizoanzishwa na Dkt. Magufuli.
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Kupitia ukurasa wake wa Instagram mjasiriamali Faiza Ally ameweka wazi hisia zake na kusema kuwa anatamani sana kuona msanii wa Bongo Flev...
-
UNAPOTAJA jina la mwanamuziki mkubwa barani Afrika, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' kutoka Tanzania, akili za wengi zinakimbilia kwe...
-
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya siku tano ya kunyesha mvua kubwa inayoweza kusababisha athari ikiwemo mafuriko. ...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Geneva, Switzerland /AFP /.More than 100 groups urged the International Labour Organization to stop taking money from tobacco companies as t...