Saturday, February 13, 2021
Waziri Mkuu Ampongeza CEO Wa Simba Kwa Ubunifu Na Uzalendo
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amempongeza Mtendaji Mkuu wa timu ya Simba mwanadada Barbra Gonzalez kwa ubunifu na uzalendo wa hali ya juu kwa kushirikisha Wizara ya Maliasili na Utalii kulitangaza Taifa kupitia jezi wanazozivaa katika mashindano ya Klabu Bingwa Afrika zilizoandikwa VISIT TANZANIA.
Pia, Waziri Mkuu amewapongeza mabingwa wa Soka Tanzania Bara, timu ya Simba kwa kushinda mchezo wake wa kwanza katika hatua ya makundi wakiwa ugenini dhidi ya Klabu ya AS Vita huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumamosi, Februari 13, 2021) wakati akiahirisha Mkutano wa Pili wa Bunge la 12, Bungeni jijini Dodoma. Amesema kitendo kilichofanywa Mtendaji Mkuu wa timu ya Simba ni cha kizalendo na kinapaswa kuigwa na timu nyingine.
Simba inayoongozwa mwanadada Barbra kama Mtendaji Mkuu wa timu hiyo, ilifanikiwa kufuzu kuingia hatua ya makundi katika mashindano ya Klabu Bingwa Afrika. Timu nyingine ya Tanzania inayoshiriki mashindano ya kimataifa ni Namungo FC ambayo inashiriki kombe la Shirikisho barani Afrika.
Pia, Waziri Mkuu amempongeza mchambuzi maarufu wa michezo nchini Ali Kamwe, ambaye kupitia ukurasa wake wa instagram, ameeleza vizuri maana ya matumizi ya neno VISIT TANZANIA na namna nchi yetu itakavyonufaika na ubunifu huo.
"Kwa mujibu wa maelezo yake, neno VISIT TANZANIA linakadiriwa kutazamwa na wapenzi wa soka takriban milioni 500 kutoka sehemu mbalimbali duniani. Wapenzi hao wa mpira kupitia vituo vya Televisheni vya Canal Algérie, BeIN Sports, Eurosport, ESPN, Arryadia, GTV ya Ghana, MENA beIN Sports na West Africa Canal+ wameshuhudia mchezo wa jana."
"Kwa lugha nyingine ni kwamba neno 'VISIT TANZANIA' lililopo sehemu ya kifuani mwa jezi ya Klabu ya Simba litaonekana kupitia chaneli hizo kwa kila dakika 90 ambazo Simba itashuka dimbani iwe dhidi ya Al-Ahly (Misri), El-Mereikh (Sudan) au dimba la nyumbani kwa Mkapa (Tanzania). Tutavuta watalii wengi kuifuatilia Nchi yetu."
Kadhalika, Waziri Mkuu amesema Tanzania imeendelea kung'ara pia kwenye medani ya masumbwi, ambapo amewapongeza mabondia Mfaume Mfaume kwa kufanikiwa kutetea ubingwa wa East and Central Africa mwezi Decemba 2020; Bondia Ibrahimu Class Mgendera kwa kushinda Ubingwa wa World Boxing Federation Intercontinental lightweight (WBF).
Vilevile, Waziri Mkuu amewapongeza bondia Tonny Rashidi aliyefanikiwa kutetea mkanda wake wa African Boxing Union (ABU) na bondia Shabani Hamadi JONGO aliyeshinda ubingwa wa WBF International Cruiserweight mwishoni mwa Januari 2021. "Bila kuwasahau Mabondia walioonesha uwezo mkubwa wa kina Hassan Mwakinyo, Twaha Kiduku na Dulla Mbabe ambaye atapanda ulingoni tarehe 26 Februari, 2021."
(Mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Wanajeshi wawili wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa wamejeruhiwa baada ya kifaru cha Israel kufyatua risasi kuelekea mnara wa Umoja wa M...
-
Katika kila makabiliano ya kijeshi kati ya Israel na Lebanon, bila kujali ni upande gani unaopigana huko Lebanon, Mto Litani, moja ya mito...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...