Friday, January 8, 2021
Trafik akamatwa kwa kuomba rushwa ya ngono akamailieshe uchunguzi
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Kilimanjaro inamshikilia Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Peter Albert Moshi kwa tuhuma za kuomba Rushwa ya Ngono.
Askari huyo alikuwa akichunguza ajali ya pikipiki ambayo ilimgonga mtoto na kusababisha kuvunjika mkono. Aliomba Rushwa Ngono kwa mama wa mtoto ili aweze kukamilisha Taarifa za Uchunguzi.
Kamanda wa TAKUKURU mkoa wa Kilimanjaro, Frida Wikesi amesema, askari huyo amekamatwa Januari 6 akiwa nyumba ya kulala wageni maeneo ya Soweto Mjini Moshi.
Uchunguzi wa TAKUKURU umebaini kuwa, Peter alimsumbua mama wa mtoto kwa muda mrefu na hivyo kusababisha shauri kuchelewa hali iliyopelekea mama huyo kupeleka malalamiko na wakaweka mtego wa kumkamata.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
