Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, amewataka wataalamu wa jiolojia nchini kutekeleza wajibu wao kwa weledi ili kuongeza mchango wa sekta ya madini kwenye pato la Taifa kutoka 5.2% mwaka 2019 hadi kufikia 10% mwaka 2025.
Mongella ametoa wito huo katika mkutano mkuu wa mwaka wa chama cha wanajiolojia nchini, unaofanyika jijini Mwanza na kushirikisha wataalamu pamoja na wadau wa jiolojia kutoka sekta mbalimbali zikiwemo za madini na nishati.
Rais wa Chama cha Wanajiolojia Tanzania, Prof. Abdulkarim Mruma, amesema ongezeko la mchango wa sekta ya madini katika pato la Taifa kutoka 3.2% mwaka 2012 hadi 5.2% mwaka jana, limetokana na hatua mbalimbali zilizochukuliwa na Serikali ikiwemo mabadiliko ya sheria zinazosimamia maliasili na rasilimali za Taifa ya mwaka 2017.
Prof. Mruma amesema usimamizi makini utawezesha sekta ya madini kuchangia 10% ya pato la Taifa ifikapo mwaka 2025.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini, James Mataragio, amesema Serikali imejipanga kusambaza nishati ya gesi asilia ili kukidhi ongezeko la mahitaji ya nishati hiyo ndani na nje ya nchi.
Kupitia mkutano huo utakaofikia tamati Novemba 29, baadhi ya wachimbaji wadogo watapata mafunzo kuhusu namna ya kuendesha uchimbaji wenye tija.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...