Monday, October 26, 2020
Wasimamizi Wa Vituo Vya Kupigia Kura, Makarani Waongozaji Wapewa Mafunzo
Msimamizi wa Uchaguzi Mkuu Jimbo la Busega Anderson Njiginya Kabuko, amewataka wasimamizi, wasimamizi wasaidizi na makarani waongozaji wa vituo vya kupigia kura katika uchaguzi mkuu kuzingatia maelekezo na mafunzo yote wanayopewa ili kufanikisha zoezi la Uchaguzi mkuu wa tarehe 28/10/2020. Kabuko ameyasema hayo wakati akifungua semina ya mafunzo tarehe 24/10/2020 katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Bulima.
Aidha amewataka wasimamizi na wasimamizi wasaidizi wa vituo kuwa makini na kutojihusisha na vitendo vitakavyowatia hatiana ikiwemo vitendo vya rushwa. "Katika kipindi hiki mnaweza kupata ushawishi mkubwa kutoka kwa makundi mbalimbali, ushawishi utakaoashiria vitendo vya rushwa, hivyo kufanya hivyo ni kinyume na taratibu za usimamizi wa Uchaguzi", aliongeza Kabuko.
Wasimamizi, wasimamizi wasaidizi na makarani waongozaji wa vituo vya kupigia kura wamekula viapo mbele ya Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Busega huku sehemu yao wakikiri kwamba mafunzo hayo yamewafanya kufahamu mambo mengi hivyo wanatarajia kufanya kazi kwa uadilifu mkubwa.
Semina ya mafunzo kwa wasimamizi wakuu wa vituo na wasimamizi wasaidizi yanafanyika kwa siku mbili kuanzia tarehe 25 hadi 26 Oktoba 2020 katika ukumbi wa Shule ya Msingi Bulima na Silsos, lakini awali pia yalifanyika mafunzo ya Makarani waongozaji wa vituo vya kupigia kura ambapo mafunzo yalifanyika tarehe 24/10/2020 katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Bulima.
Jumla ya wasimamizi wakuu, wasimamizi wasaidizi na makarani waongozaji wapatao 1,300 watashiriki katika Uchaguzi wa mkuu katika jumla ya vituo 325 jimbo la Busega.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
