Wednesday, June 10, 2020
Wabunge 69 wa CHADEMA Kuhojiwa Leo na Takururu.....
Na Ezekiel Mtonyole, Dodoma.
Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa TAKUKURU Makao makuu Dodoma, leo inatarajia kuanza kuwahoji Wabunge na waliokuwa Wabunge wa chama Cha Demokrasia na Maendeleo kwa tuhuma mbalimbali zinazowakabili.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TAKUKURU inasema wabunge hao watahojiwa kutokana na tuhuma mbalimbali ambazo zimetolewa na baadhi ya wabunge ambao wamehama chama hicho na kudai kuna fedha walikuwa wakichangishwa lakini matumizi yake hayajulikani.
"Tunapenda kuthibitishia umma kwamba ni kweli kuwa TAKUKURU Makao makuu imewaita waheshimiwa wabunge wa CHADEMA na waliowahi kuwa wabunge wa chama hicho kwa mahojiano" imesema taarifa hiyo.
Taarifa hiyo inasema mahojiano hayo ni mwendelezo wa uchunguzi unaoendeshwa na TAKUKURU Makao makuu wa malalamiko dhidi ya matumizi ya fedha za chama na hatua ya Sasa ni kuhoji wabunge sitini na tisa(69).
Kwa mujibu wa malalamiko hayo wabunge hao wanadai walikuwa wakikatwa kwa wabunge viti maalumu walikuwa wakikatwa kiasi Cha milioni moja laki tano na sitini(1,560,000) na wabunge wa kuchaguliwa walikuwa wakikatwa laki tano na ishirini (520,000).
Na wabunge hao walidai kutojua matumizi ya fedha hizo, na kwa mujibu wa taarifa ya Mkurugenzi wa TAKUKURU Brigedia Jenarali John Mbungo, Mei 27, 2020 kwamba uchunguzi tayari ulishaanza na baadhi ya viongozi wameshahojiwa.
Kwa mujibu wa taarifa ya TAKUKURU yataanza kufanyika leo TAKUKURU Makao Mkuu Dodoma na yanatarajiwa kukamilika wiki ijayo
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
