Wednesday, June 10, 2020
Wabunge 69 wa CHADEMA Kuhojiwa Leo na Takururu.....
Na Ezekiel Mtonyole, Dodoma.
Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa TAKUKURU Makao makuu Dodoma, leo inatarajia kuanza kuwahoji Wabunge na waliokuwa Wabunge wa chama Cha Demokrasia na Maendeleo kwa tuhuma mbalimbali zinazowakabili.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TAKUKURU inasema wabunge hao watahojiwa kutokana na tuhuma mbalimbali ambazo zimetolewa na baadhi ya wabunge ambao wamehama chama hicho na kudai kuna fedha walikuwa wakichangishwa lakini matumizi yake hayajulikani.
"Tunapenda kuthibitishia umma kwamba ni kweli kuwa TAKUKURU Makao makuu imewaita waheshimiwa wabunge wa CHADEMA na waliowahi kuwa wabunge wa chama hicho kwa mahojiano" imesema taarifa hiyo.
Taarifa hiyo inasema mahojiano hayo ni mwendelezo wa uchunguzi unaoendeshwa na TAKUKURU Makao makuu wa malalamiko dhidi ya matumizi ya fedha za chama na hatua ya Sasa ni kuhoji wabunge sitini na tisa(69).
Kwa mujibu wa malalamiko hayo wabunge hao wanadai walikuwa wakikatwa kwa wabunge viti maalumu walikuwa wakikatwa kiasi Cha milioni moja laki tano na sitini(1,560,000) na wabunge wa kuchaguliwa walikuwa wakikatwa laki tano na ishirini (520,000).
Na wabunge hao walidai kutojua matumizi ya fedha hizo, na kwa mujibu wa taarifa ya Mkurugenzi wa TAKUKURU Brigedia Jenarali John Mbungo, Mei 27, 2020 kwamba uchunguzi tayari ulishaanza na baadhi ya viongozi wameshahojiwa.
Kwa mujibu wa taarifa ya TAKUKURU yataanza kufanyika leo TAKUKURU Makao Mkuu Dodoma na yanatarajiwa kukamilika wiki ijayo
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
