Wednesday, June 10, 2020
Wabunge 69 wa CHADEMA Kuhojiwa Leo na Takururu.....
Na Ezekiel Mtonyole, Dodoma.
Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa TAKUKURU Makao makuu Dodoma, leo inatarajia kuanza kuwahoji Wabunge na waliokuwa Wabunge wa chama Cha Demokrasia na Maendeleo kwa tuhuma mbalimbali zinazowakabili.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TAKUKURU inasema wabunge hao watahojiwa kutokana na tuhuma mbalimbali ambazo zimetolewa na baadhi ya wabunge ambao wamehama chama hicho na kudai kuna fedha walikuwa wakichangishwa lakini matumizi yake hayajulikani.
"Tunapenda kuthibitishia umma kwamba ni kweli kuwa TAKUKURU Makao makuu imewaita waheshimiwa wabunge wa CHADEMA na waliowahi kuwa wabunge wa chama hicho kwa mahojiano" imesema taarifa hiyo.
Taarifa hiyo inasema mahojiano hayo ni mwendelezo wa uchunguzi unaoendeshwa na TAKUKURU Makao makuu wa malalamiko dhidi ya matumizi ya fedha za chama na hatua ya Sasa ni kuhoji wabunge sitini na tisa(69).
Kwa mujibu wa malalamiko hayo wabunge hao wanadai walikuwa wakikatwa kwa wabunge viti maalumu walikuwa wakikatwa kiasi Cha milioni moja laki tano na sitini(1,560,000) na wabunge wa kuchaguliwa walikuwa wakikatwa laki tano na ishirini (520,000).
Na wabunge hao walidai kutojua matumizi ya fedha hizo, na kwa mujibu wa taarifa ya Mkurugenzi wa TAKUKURU Brigedia Jenarali John Mbungo, Mei 27, 2020 kwamba uchunguzi tayari ulishaanza na baadhi ya viongozi wameshahojiwa.
Kwa mujibu wa taarifa ya TAKUKURU yataanza kufanyika leo TAKUKURU Makao Mkuu Dodoma na yanatarajiwa kukamilika wiki ijayo
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Kupitia ukurasa wake wa Instagram mjasiriamali Faiza Ally ameweka wazi hisia zake na kusema kuwa anatamani sana kuona msanii wa Bongo Flev...
-
UNAPOTAJA jina la mwanamuziki mkubwa barani Afrika, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' kutoka Tanzania, akili za wengi zinakimbilia kwe...
-
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya siku tano ya kunyesha mvua kubwa inayoweza kusababisha athari ikiwemo mafuriko. ...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Geneva, Switzerland /AFP /.More than 100 groups urged the International Labour Organization to stop taking money from tobacco companies as t...