Ugiriki na Israel zimepanga kushirikiana kwenye kurejea upya kwa shughuli za utalii kati yao katika mwezi Agosti, huku zikieleza wasiwasi wao juu ya hatua ya Uturuki kuanza utafutaji mafuta na gesi kwenye eneo la mashariki mwa Mediterenia.
Waziri Mkuu wa Ugiriki, Ky-ria-kos Mit-so-takis, ambaye yuko kwenye ziara yake ya kwanza nje ya nchi tangu kuanza kwa janga la COVID-19, amefanya mazungumzo na mwenyeji wake, Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, mjini Tel Aviv, kuhusiana na mpango wa nchi zao pamoja na Cyprus kusaka gesi asilia na utalii.
Ugiriki ilifunguwa milango yake jana Jumatatu kwa wasafiri wa Umoja wa Ulaya. Israel, ambayo raia wake milioni 1.2 hutembelea Ugiriki kila mwaka, ni soko kubwa kwa taifa hilo la Ulaya.
Netanyahu amesema kwamba kuanzia tarehe 1 Agosti, wageni kutoka Ugiriki hawatalazimika kujiweka karantini ya siku 14 kama ilivyo sasa.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
