Kaptein wa Zamani wa Timu ya vijana ya Zanzibar na Mchezaji mkongwe visiwani Zanzibar, Hashim Salum Hashim amejitokeza kuchukua fomu ya kuwania nafasi ya Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi CCM.
Hashim Salum Hashim anakuwa mgombea 24 kufika katika ofisi kuu za chama hicho zilizopo kisiwandui mjini Unguja na kukabidhiwa fomu na katibu Katibu wa Kamati Maalumu ya NEC,Idara ya organization Zanzibar Cassian Galos Nyimbo.
Hashim Salum Hashim alivuma kisoka katika miaka ya 90 na timu aliochezea ni Timu ya mpira wa miguu ya Miembeni iliyopo katikati ya viunga vya Zanzibar, Hashim alipata umaarufu kwa kuwa mchezaji mwenye mashuti vusiwani humo.
Mara bbaada ya zoezi la uchukuaji wa Fomu, Hashim Salum Hashim aliwaambia waandishi wa Habari kwamba pindipo chama cha Mapinduzi kitampa ridhaa ya kuwa mgombea pekee wa nafasi ya Urais wa Zanzibar na Wananchi kumchagua ataanza kuboresha michezo hususani katika soka la vijana.
Alisema lengo lake ni kurudisha hadhi ya soka visiwani Zanzibar kama ilivyokuwa awali katika miaka ya 80s hadi miaka ya 90.
Hata hivyo alisema kwamba pindipo atakuwa rais wa Zanzibar, Serikali yake itatoa ufadhili wa michezo kwa asilimia kubwa ili kurudisha hadhi ya Sekta hiyo visiwani humo.
"Mimi kipaumbele kikubwa changu ni kutekeleza masuala ya michezo kutokana na kuwa mimi ni mwana michezo kama Mungu akijalia nikiwa Rais nitahakikisha michezo inapata wadhamini kwa asilimia 100 kutoka katika serikali,"alisema
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
