Kaptein wa Zamani wa Timu ya vijana ya Zanzibar na Mchezaji mkongwe visiwani Zanzibar, Hashim Salum Hashim amejitokeza kuchukua fomu ya kuwania nafasi ya Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi CCM.
Hashim Salum Hashim anakuwa mgombea 24 kufika katika ofisi kuu za chama hicho zilizopo kisiwandui mjini Unguja na kukabidhiwa fomu na katibu Katibu wa Kamati Maalumu ya NEC,Idara ya organization Zanzibar Cassian Galos Nyimbo.
Hashim Salum Hashim alivuma kisoka katika miaka ya 90 na timu aliochezea ni Timu ya mpira wa miguu ya Miembeni iliyopo katikati ya viunga vya Zanzibar, Hashim alipata umaarufu kwa kuwa mchezaji mwenye mashuti vusiwani humo.
Mara bbaada ya zoezi la uchukuaji wa Fomu, Hashim Salum Hashim aliwaambia waandishi wa Habari kwamba pindipo chama cha Mapinduzi kitampa ridhaa ya kuwa mgombea pekee wa nafasi ya Urais wa Zanzibar na Wananchi kumchagua ataanza kuboresha michezo hususani katika soka la vijana.
Alisema lengo lake ni kurudisha hadhi ya soka visiwani Zanzibar kama ilivyokuwa awali katika miaka ya 80s hadi miaka ya 90.
Hata hivyo alisema kwamba pindipo atakuwa rais wa Zanzibar, Serikali yake itatoa ufadhili wa michezo kwa asilimia kubwa ili kurudisha hadhi ya Sekta hiyo visiwani humo.
"Mimi kipaumbele kikubwa changu ni kutekeleza masuala ya michezo kutokana na kuwa mimi ni mwana michezo kama Mungu akijalia nikiwa Rais nitahakikisha michezo inapata wadhamini kwa asilimia 100 kutoka katika serikali,"alisema
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...