Mwanamuziki wa kimataifa wa miondoko aina ya R&B na Pop Justine Bieber amekanusha madai ya ubakaji yaliyojitokeza kwenye mtandao wa Twitter kupitia akaunti ya mtu asiyejulikana.
Watu wawili wasiojulikana walituma ujumbe kwa njia ya Twitter wakidai kwamba unyanyasaji huo ulitokea mwaka 2014 na 2015.
Akaunti ya mshtaki ambaye hajulikani imeondolewa kwenye mtandao wa Twitter lakini Justin Bieber amejibu na kusema: "Madai haya hayana ukweli wowote."
Akaunti ya pili bado ipo kwenye mtandao huo wa Twitter. Akaunti hii mwenyewe anajulikana.
Msemaji wa Justin Bieber amezungumza na Newsbeat ya BBC na kusema kwamba hakuna anachoweza kusema kuhusu madai hayo na kwamba hana cha kuongeza katika akaunti ya mtandao wa Twitter ya mwimbaji huyo.
Justin Bieber alijibu madai hayo baada kuzungumza na mke wake na timu yake ambayo aliyakanusha vikali.
Katika msururu wa ujumbe kwenye Twitter, mwimbaji huyo alituma picha kutoka kwa simu yake na ujumbe kuanzia usiku ambao unadaiwa madai hayo yalitokea 2014, ambao unaonesha mawasiliano yake na aliyekuwa mchumba wake Selena Gomez.
Anasema kwamba wao hawakuwahi kuishi katika hoteli ya Four Seasons lakini alikuwa kwenye makazi ya kampuni ya AirBnB na marafiki zake.
Pia, ametuma picha za ujumbe unaodai kwamba alionekana hoteli ya Four Seasons Machi 10, siku moja baada ya madai ambayo yanasemekana unyanyasaji huo ulitokea. Akaunti hiyo ya Twitter inaonekana kuwa imeondolewa.
Newsbeat imezungumza na hoteli ya Four Seasons kutaka maoni yao.
Justin Bieber pia ameoesha ujumbe kwenye barua yake pepe na risiti za kampuni ya AirBnB na hoteli ya Westin alikokuwa siku ambazo zimetiwa doa.
Anasema alikuwa anatumia majina ambayo sio ya kweli ya Mike Lowery.
Justin Bieber bado hajajibu shutuma za mtu wa pili ambaye anajulikana kwa jina la Kadi, anayedai kuwa alimnyanyasa katika hoteli ya New York Mei 2015.
Newsbeat imezungumza na mwakilishi wake kutaka maoni yake kuhusiana na madai hayo ya pili.
Source
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
