Thursday, April 23, 2020
"Wagonjwa wa Corona Walitaka Kutoroka" - DC Ilala
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema, amesema kuwa bado hajapata taarifa za waathirika wa Virusi vya Corona, waliopo katika kituo maalum katika Hospitali ya Amana, kama wametoroka na kurejea makwao ila anachojua walikuwa wanatishia kuondoka kwa madai ya kuwa hali zao kiafya ni nzuri.
Mjema ameyabainisha hayo leo Aprili 23,2020, wakati akizungumza na ITV, kufuatia taarifa mbalimbali zilizokuwa zikisambaa kwenye mitandao ya kijamii zikieleza kuwa, baadhi ya wagonjwa katika hospitali hiyo wameleta vurugu na wengine kutoroka.
"Bado hatuna taarifa ya wagonjwa katika Hospitali ya Amana waliotoroka na kupanda daladala kurejea makwao, ngoja tuifuatilie ila tunachojua ni kwamba walikuwa wanasema wanataka kurudi nyumbani, kifupi walikuwa wanatishia tu" DC Ilala, Sophia Mjema.
Aidha DC Mjema ameongeza kuwa "Kulikuwa na wagonjwa ambao walikuwa wamefika pale na kusema kuwa wao hawaumwi sana kwahiyo walikuwa wanataka waruhusiwe na unajua ukifika pale, ukiwa mshukiwa lazima ukae kidogo hospitali uangaliwe wakuone upo vizuri ndiyo uruhusiwe".
EATV&EA Radio Digital, ilimtafuta Mkuu huyo wa Wilaya kwa ajili ya kupanda undani wa taarifa hizo, ambapo alidai kuwa yupo kwenye kikao na akitoka basi atatupigia simu na kutueleza ni kipi kilichojiri na hatua zipi ambazo zimekwishachukuliwa hadi sasa.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
