Thursday, April 2, 2020
RC Tabora Awaagiza Kusakwa Na Kukamatwa Kwa Walimu Wanaofundisha Tuisheni Kipindi Hiki Cha Mapambano Dhidi Ya Corona
Na Daudi Tiganya
MKUU wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri ameagiza kuwasakwa kwa walimu ambao wamekuwa wakiwakusanya wanafunzi kwa ajili ya kufundisha tuisheni kwa kuwa wanapingana na kampeni ya kudhibiti na kupambana na ugonjwa wa Covid -19.
Hatua hiyo inalenga kuzuia vitendo hatarishi vinavyoweza kuwepo na mazingira kupata virusi vya Corona.
Mwanri alitoa kauli hiyo wilayani Nzega wakati ziara yake ya kukagua Vituo na Zahanati zilizoandaliwa kwa ajili ya washukiwa wa ugonjwa wa covid -19 kama itatokea bahati wakaonekana wakaonekana Mkoani humo.
Alisema ni marufuku kwa walimu kutumia janga la ugonjwa wa Covid -19 kujipatia maslahi kwa kufanya hivyo ni kuvunja Sheria kwa kisingizio kuwa wanawafundisha watoto masomo ya ziada.
Mwanri aliongeza kuwa baadhi ya Wamiliki wa Shule binafsi ndio wanasababisha walimu kujiingiza kwenye ufundishaji wa tuisheni baada ya kusema kuwa kuambiwa kuwa hatawalipa mshahara kwa sababu hawakufundisha katika kipindi ambao shule zimefungwa kutokana na Covid -19.
Alisema hilo halikubaliki na ndio linalowafanya baadhi yao kujiingiza katika ufundishaji wa tuisheni kinyume cha maagizo ya serikali katika kukabiliana na Covid 19.
Mwanri alisema ni lazima walimu wote walipwe mshahara wao ili kutowaweka katika vishawishi vya kujiingiza katika kuvunja maagizo ya Serikali ya kuzuia mikusanyiko kwa wanafunzi.
Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt. Honaratha Rutatinisibwa aliwataka wazazi kutowaruhusu watoto wao kuzuzura ovyo mitaani kwa kuwa vitendo vinaweza kuwasababisha kupata maambukizi ya virusi vya Corona.
Alisema kuna baadhi ya maeneo kunaonekana makundi ya watoto wakiwa wamekusanyika pamoja jambo ambalo ni hatari kwao na kwa jamii zinazowazunguka.
Dkt. Rutatinisibwa alisema ni vema wanafunzi wakasisitizwa kubaki majumbani katika kipindi hiki ambacho mapambano dhidi ya Corona yakiendelea
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
