Saturday, April 4, 2020
Eto'o Awajia Juu Maprofesa Wa Ulaya kuhusu chanjo ya COVID-19 kufanyiwa majaribio Afrika
Supastaa wa zamani wa Inter Milan na Chelsea, Samuel Eto'o amewatolea uvivu maprofesa nchini Ufaransa kufuatia matamshi yao yasiyofaa juu ya Afrika kipindi hiki ambacho ulimwengu unatafuta ufumbuzi dhidi ya kupambana na ugonjwa wa Virusi vya Corona.
Hakuna dawa ambazo zinaweza kuzuia ugonjwa huu, lakini wanasayansi wamegundua chanjo ya BCG, inayotumika kupunguza makali ya ugonjwa huo.
Kupitia kituo cha televisheni cha Ufaransa LCI, Profesa Jean-Paul Mira, mkuu wa kitengo cha huduma ya wagonjwa katika hospitali ya Cochin (Paris) na Profesa Camille Locht, mkurugenzi wa utafiti huko Inserm alipendekeza ufanisi wa chanjo hiyo inapaswa kufanyiwa majaribio Afrika.
Kauli hiyo, ilimchukiza Eto'o na kutumia mtandao wake wa kijamii kwa kuandika. "Afrika sio uwanja wako wa kucheza."
Nyota wa kimataifa wa Senagel, Demba Ba, alionekana kukerwa na msomi huyo kwa kuandika, "Karibu Magharibi, ambapo watu weupe wanajiamini kuwa bora zaidi kwamba ubaguzi wa rangi na ujasusi huwa kawaida. Wakati wa kuinuka."
Kiungo wa zamani wa Ufaransa na kiungo wa Inter Milan, Olivier Dacourt alionyesha msimamo wake katika Twitter.
"Je! Ni kweli wapo siriazi?" aliuliza.
Kuna watu wamekuwa wakikimbilia Ulaya ili wasaidiwe kisiasa lakini hivi ndivyo wazungu wanavyotuchukulia
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
