Thursday, April 18, 2019
RC Mara atoa agizo katika halmashauri kuhusu zao la kahawa
Na Timothy Itembe, Mara
Mkuu wa mkoa Mara,Adamu Kigoma Malima amezitaka halmashauri zake 05 zinazojishugulisha na kilimo cha zao la kahawa kuhakikisha kilimo hicho kinapanda kutoka Tani 2000 hadi kufika Tani 3200 kwa mwaka ifikapo mwaka 2022.
Malima aliongeza kuwa mkakati mwingine wa mkoa Mara katika zao la kahawa ni kuhakikisha kuwa Mara chini ya mwavuli wa wenyeji wake wilaya Tarime wanalima Kahawa kwa wingi na yenye Ubora ili kuwavutia wanunuzi na kuongeza kipato.
"Tunahitaji kilimo cha kisasa chenye tija ili kuongeza wingi na ubora wa Kahawa kwa hali hiyo tunatarajia kuwa na soko la kahawa hapa hapa Tarime badala ya kusumbuka kwenda kutafuta Masoko nje ya Tarime kwa hali hiyo tutakuwa tumepunguza garama za usafirishaji ambazo zinatutesa huku tukipata fedha kidogo ya kuendeshea shuguli za maendeleo ikiwemo ya kifamilia"alisema Malima.
Malima alitumia nafasi hiyo kuzitaka halimashauri hizo ambazo ni Tarime,Butiama,Bunda,Serengeti na Rorya chini ya mwavuli wa wenyeji wao wilaya Tarime kuandika andiko la kuomba mkopo wa fedha ifikapo Aprili 30 kutoka ndani ya Benki ya TADB ili kuongeza jitihada za kilimo cha kahawa kutoka tani zilizopo hadi kufikia malengo waliojiwekea ndani ya miaka 05.
Kwa upande wake moja wa Bodi ya kahawa,Melkiad Masawe alisema kuwa kazi ya bodi ni kutafuta masoko na kuwa ili wakulima waweze kunufaika na kilimo cha kahawa ni sharti walime kwa kuzingatia kanuni za kilimo pamoja na wakulima kujiandikisha katika Daftari la kilimo hai.
Masawe aliongeza kuwa changamoto wanayo kumbana nayo nipamoja na Bei ya kahawa kushuka sokoni na kusababisha wakulima kukata tama katika kilimo cha kahawa kiasi kwamba fedha wanayopata haikidhi mahiyaji.
Mwenyeji wa kikao hicho cha wadau wa zao la wakahawa ambacho kilifanyikia Nyamwaga wilayani Tarime ili kujadili mkakati wa kufikia lengo la Tani 5000 ifikapo mwaka 2022,Afisa kilimo na Umwagiliaji wilaya Tarime,Sluvanus Gwiboha alisema kuwa kuhakikisha kuwa lengo linafikiwa sharti wakulima wapande kahawa ya Vikonyo.
Mkakati uliopo kwa halmashauri ya Tarime ni kuzalisha kahawa kwanjia ya vikonyo na Mbegu ili kuongeza uzalishaji kwa eneo kutoka tani 0.8 hadi tani 1.5 kwa heka,kuongeza uzalishaji wa kahawa kutoka tani 2000 hadi tani 3200 kwa mwaka,kuandaa vitalu vitatu vitakavyozalisha miche 1,005,000 ifikapo 2021/2022.
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Mara nyingi wanawake wamekuwa watu wa kukaa kimya bila kusema wanataka nini ili kuridhishwa katika mapenzi na mbaya zaidi katika swala zima ...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...

