Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Kasheku (Musukuma) ameitaka Wizara ya Katiba na Sheria kufanya marekebisho ya baadhi ya sheria zinazoonekana hazina manufaa kwa mazingira ya sasa.
Musukuma ametoa kauli hiyo katika vikao vya Bunge kwenye mjadala wa Wizara ya Katiba na Sheria ambapo kupitia Waziri wa Katiba na Sheria, Agustino Mahiga aliwasilisha makadirio ya bajeti yake.
"Niseme tu kiukweli ni vizuri mkaangalia mkarekebisha sheria, hasa kwenye makosa madogodogo ambayo yamepelekea magereza mengi kujaa mahabusu ambayo kwa kweli mengine yanastahili makofi tu mtu akaenda nyumbani", amesema.
Musukuma ameongeza kuwa, "nashauri sana hizi sheria zilizotungwa tukiwa milioni 20, leo tuko milioni 55 mtu anawekwa wiki 2 kwa kesi ya kuiba kuku, ni vitu ambavyo tufikirie adhabu ili kupunguza mrundikano wa mahabusu kule ndani."
"Nilisoma kwenye kitabu cha Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kuhusiana na uteuzi wa Majaji, inampa mamlaka Rais kuteua na anakuwa jopo la kumshauri ninawataka tu wenzangu wamuachie Rais akafanya majukumu yake." amemalizia Musukuma.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
