Usiku wa jana, Machi 24 imeshuhudiwa historia kubwa katika Uwanja wa Taifa ambapo timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars imefuzu michuano ya Mataifa ya Afrika AFCON baada ya miaka 39.
Hiyo ni baada ya kuifunga timu ya taifa ya Uganda 'The Cranes" kwa mabao 3-0, mabao yaliyofungwa na Simon Msuva, Erasto Nyoni na Aggrey Morris.
Nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta ni miongoni mwa wachezaji waliocheza kwa kiwango cha juu katika mchezo huo, mara baada ya kumalizika kwa mchezo alikwea pipa na kurejea Ubelgiji katika klabu yake ya Genk huku akiacha ujumbe mzito kwa Watanzania.
Najivunia ubora uliooneshwa na wachezaji wenzangu,najivunia uwepo wa benchi la ufundi likiongozwa na kocha amunike, najivunia uwepo wa mashabiki waliojitokeza kutusapoti katika mchezo wetu wa jana na najivunia kuwa mtanzania na kapteni wa timu yangu ya taifa. Asanteni wote mliohamasisha na wote mliojotokeza kutusapoti
A post shared by Mbwana Samatta (@samagoal77) on Mar 24, 2019 at 4:42pm PDT
Pia wakati anaondoka katika Uwanja wa Ndege wa JNIA kuelekea Ubelgiji, majira ya saa 7 za usiku, Samatta aaliandika ujumbe, "mpaka wakati ujao, ahsanteni sana", ukionesha kuwa yuko safarini kurejea klabuni kwake.
Taifa Stars imeungana na timu ya taifa ya Uganda, Kenya na Burundi zitakazoiwakilisha Afrika Mashariki katika michuano ya AFCON itakayofanyika kuanzia mwezi June hadi Julai, 2019 nchini Misri.
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Wanajeshi wawili wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa wamejeruhiwa baada ya kifaru cha Israel kufyatua risasi kuelekea mnara wa Umoja wa M...
-
Katika kila makabiliano ya kijeshi kati ya Israel na Lebanon, bila kujali ni upande gani unaopigana huko Lebanon, Mto Litani, moja ya mito...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...