Waziri Mkuu Mstaafu na aliyekuwa Mwenyekiti wa Rasimu ya Katiba, Jaji Joseph Sinde Warioba amewashauri viongozi na wanasiasa vijana waliopo madarakani kuwa na maadili katika kazi zao na kwamba wakumbuke kuna maisha baada ya uongozi.
Jaji warioba ameyasema hayo wakati akifanya mahojiano maalumu na www.eatv.tv ambapo amesema kwamba wakati wa kupumzika kama mstaafu unapaswa kupumzika ukiwa na amani ya moyo.
Jaji Warioba ameeleza kwamba yeye wakati alipokuwa kazini alikuwa na ushirikiano na wananchi lakini alipotoka madarakani ndipo aliposhuhudia namna gani wananchi walivyokuwa wakimuheshimu jambo ambalo linamfariji kwa sasa akiwa kwenye mapumziko yake.
Amesema kwamba ili vijana wa sasa waweze kupata heshima ambayo yeye anapatiwa na watanzania, wanapaswa kuwatumikia wananchi kwa moyo mmoja bila kuwa na makandokando yoyote na siyo kuangalia sifa wanazopewa kwa sasa wakiwa kwenye uongozi.
"Nachowashauri vijana waliopo kwenye uongozi, wawatumikie wananchi kwa moyo mmoja. Wanapotoka madarakani wakumbuke kuna maisha mengine yataendelea. Mimi ninafurahi heshima wanayonipa watanzania kwa sasa. Hakuna kitu kizuri kama kuwa na amani ya moyo wakati ukishakuwa umestaafu", amesema mzee Warioba.
"Kwa sasa wakiwa viongozi wanaweza kuwa wanasifiwa lakini ukipewa heshima ukiwa umestaafu ni nzuri kwakuwa tayari unakuwa kwenye maisha mengine," ameongeza.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
