Waziri Mkuu Mstaafu na aliyekuwa Mwenyekiti wa Rasimu ya Katiba, Jaji Joseph Sinde Warioba amewashauri viongozi na wanasiasa vijana waliopo madarakani kuwa na maadili katika kazi zao na kwamba wakumbuke kuna maisha baada ya uongozi.
Jaji warioba ameyasema hayo wakati akifanya mahojiano maalumu na www.eatv.tv ambapo amesema kwamba wakati wa kupumzika kama mstaafu unapaswa kupumzika ukiwa na amani ya moyo.
Jaji Warioba ameeleza kwamba yeye wakati alipokuwa kazini alikuwa na ushirikiano na wananchi lakini alipotoka madarakani ndipo aliposhuhudia namna gani wananchi walivyokuwa wakimuheshimu jambo ambalo linamfariji kwa sasa akiwa kwenye mapumziko yake.
Amesema kwamba ili vijana wa sasa waweze kupata heshima ambayo yeye anapatiwa na watanzania, wanapaswa kuwatumikia wananchi kwa moyo mmoja bila kuwa na makandokando yoyote na siyo kuangalia sifa wanazopewa kwa sasa wakiwa kwenye uongozi.
"Nachowashauri vijana waliopo kwenye uongozi, wawatumikie wananchi kwa moyo mmoja. Wanapotoka madarakani wakumbuke kuna maisha mengine yataendelea. Mimi ninafurahi heshima wanayonipa watanzania kwa sasa. Hakuna kitu kizuri kama kuwa na amani ya moyo wakati ukishakuwa umestaafu", amesema mzee Warioba.
"Kwa sasa wakiwa viongozi wanaweza kuwa wanasifiwa lakini ukipewa heshima ukiwa umestaafu ni nzuri kwakuwa tayari unakuwa kwenye maisha mengine," ameongeza.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
