Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Jerry Muro ameungana na Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Dkt Reginald Mengi, familia, ndugu, jamaa na marafiki kuupokea mwili wa mmoja wa waanzilishi wa makampuni ya IPP Mama Mercy Anna Mengi katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).
Mwili huo umewasili leo majira ya Saa 4 asubuhi katika uwanja wa ndege wa KIA ukitokea jijini Dar es salaam na kupelekwa nyumbani kwa marehemu maeneo ya Shanty Town ambako ibada fupi yakuombea mwili wa marehemu ilifanyika na kuongozwa na Mchungaji Meena wa Kanisa la KKKT Usharika wa Moshi Mjini.
Mchungaji Meena amesema ndugu na marafiki wanapotafakari safari ya mwisho ya Mama Mercy Anna Mengi watambue njia hiyo aliyopita kila mtu atapita hivyo jambo kubwa ni kuimarika katika imani na kuendelea kuishi katika maisha ya ushuhuda na kusaidia wengine bila kuogopa wala hofu kwakuwa Mungu atazidi kuwaimarisha.
Mwili wa mama Mercy Anna Mengi unatarajiwa kuagwa kwa mara ya mwisho hapo kesho baada ya ibada itakayofanyika katika Kanisa la KKKT usharika wa Moshi Mjini na kisha kupelekwa kuhifadhiwa kwenye nyumba yake ya milele katika mahala palipotengwa na wanafamilia.
Source
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mjini Richard Kasesela Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mjini Richard Kasesela amelishauri Kanisa la Kiinjili la Kilutheri ...
