Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Jerry Muro ameungana na Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Dkt Reginald Mengi, familia, ndugu, jamaa na marafiki kuupokea mwili wa mmoja wa waanzilishi wa makampuni ya IPP Mama Mercy Anna Mengi katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).
Mwili huo umewasili leo majira ya Saa 4 asubuhi katika uwanja wa ndege wa KIA ukitokea jijini Dar es salaam na kupelekwa nyumbani kwa marehemu maeneo ya Shanty Town ambako ibada fupi yakuombea mwili wa marehemu ilifanyika na kuongozwa na Mchungaji Meena wa Kanisa la KKKT Usharika wa Moshi Mjini.
Mchungaji Meena amesema ndugu na marafiki wanapotafakari safari ya mwisho ya Mama Mercy Anna Mengi watambue njia hiyo aliyopita kila mtu atapita hivyo jambo kubwa ni kuimarika katika imani na kuendelea kuishi katika maisha ya ushuhuda na kusaidia wengine bila kuogopa wala hofu kwakuwa Mungu atazidi kuwaimarisha.
Mwili wa mama Mercy Anna Mengi unatarajiwa kuagwa kwa mara ya mwisho hapo kesho baada ya ibada itakayofanyika katika Kanisa la KKKT usharika wa Moshi Mjini na kisha kupelekwa kuhifadhiwa kwenye nyumba yake ya milele katika mahala palipotengwa na wanafamilia.
Source
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Kupitia ukurasa wake wa Instagram mjasiriamali Faiza Ally ameweka wazi hisia zake na kusema kuwa anatamani sana kuona msanii wa Bongo Flev...
-
UNAPOTAJA jina la mwanamuziki mkubwa barani Afrika, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' kutoka Tanzania, akili za wengi zinakimbilia kwe...
-
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya siku tano ya kunyesha mvua kubwa inayoweza kusababisha athari ikiwemo mafuriko. ...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Geneva, Switzerland /AFP /.More than 100 groups urged the International Labour Organization to stop taking money from tobacco companies as t...