Thursday, November 8, 2018
Mwandishi wa Kenya na Afrika kusini waachiwa huru
Kufuatia kusambaa kwa taarifa kuhusu Wawakilishi wawili wa kamati ya kimataifa ya kuwalinda waandishi wa habari CPJ waliokuwa wamekamatwa nchini Tanzania wameachiwa huru kwa mujibu wa Taarifa kutoka serikali ya Afrika Kusini.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kuchapishwa kwenye tovuti ya CPJ, afisa mmoja aliyejitambulisha kuwa ni mfanyakazi wa Idara ya Uhamiaji aliwakamata wafanyakazi hao wawili wa CPJ Angela Quintal na Muthoki Mumo, katika hotel waliyofikia jijini Dar es Salaam ambapo walikagua vitu walivyokuwa navyo na baadae kuchukua pasi zao za kusafiria.
Taarifa hiyo ilidai wafanyakazi hao ambao wamekuja nchini kwa masuala ya kikazi, inaelezwa kuwa waliondolewa hotelini na kupelekwa sehemu wasioijua.
Mkurugenzi mtendaji wa CPJ Joel Simon awali alisema walikuwa na wasiwasi na usalama wa wafanyakazi wao huku wakidai kuwa waliingia Tanzania ki uhalali.
Alitoa wito kwa mamlaka nchini Tanzania kuwaachia na kuwarejeshea pasi zao za kusafiria.
"Ni jambo la kutia wasiwasi mkubwa kuwa huenda simu ya Angela Quintal imetumiwa bila idhini yake. Hatujawasiliana na Angela Quintal au Muthoki Mumo tangu wakamatwe na tunaamini kuwa wote wanazuiliwa na mamlaka za Tanzania," Joel Simon aliandika kwenye Twitter.
Hata hivyo akizungumza kwa njia ya simu afisa habari wa Idara ya Uhamiaji nchini Tanzania Ali Mtanda amesema hana habari kuhusiana na taarifa hiyo na kwamba bado hazikuwa zimefika makao makuu na kutaka kupewa muda, ili kuweza kuthibitisha.
Baada ya taarifa hiyo msemaji mkuu wa serikali ya jamhuri ya muungano wa tanzania kupitia ukurasa wake wa twitter ameandika kuwa wanafatilia kujua sababu ya waandishi hao wa CPJ waliruhusiwa kuingia nchini na baadae kuhojiwa na uhamiaji na hatimaye kuachiwa huru.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...


