Friday, November 16, 2018

Haji Manara Amtupia Dongo Shafii Dauda ''Najua Uliomba Kazi Wasafi TV Wakakuchomolea’'

Haji Manara Amtupia Dongo Shafii Dauda ''Najua Uliomba Kazi Wasafi TV Wakakuchomolea''
Baada ya tetesi kuwa kiungo mshambuliaji wa klabu ya Simba, Haruna Niyonzima yupo mbioni kujiunga na matajiri Azam FC, Hatimaye tetesi hizo zimeibua vita ya maneno kati ya Msemaji wa Simba, Haji Manara na Mchambuzi wa Soka wa kituo cha redio cha Clouds FM, Shaffih Dauda.

Shaffih Dauda kupitia ukurasa wake wa Instagram aliposti picha ya Niyonzima akiwa amevaa jezi moja iliyowekwa rangi ya Simba na Azam FC na kisha kuiandikia maneno yaliyosomeka "Kwani kuna habari gani?"



Baada ya hapo, Haji Manara aliona sio kesi akaamua kumjibu Shaffih kwa kuandika ujumbe mzito huku akimshambulia mchambuzi huyo kuwa anatumika na ni adui mkubwa wa Simba.

"Tunajua Shaffih unatumika na Maadui wa Simba kutaka kutuvuruga kusudi ili kubalance na cc tuonekane tuna mgogoro na wachezaji wetu!!. Hatuna Niyonzima yupo camp now na leo atacheza ikimpendeza kocha dhidhi ya Bata Bullets, Hivi mtu muungwana kabisa unawezaje kuandika uongo na kufikia kumvalisha jezi ya team nyingine mchezaji aliye na mkataba na klabu yetu kama c uchochezi na uhuni wa kishamba?,"ameandika Haji Manara.

Akiendelea kutupa madogo kwa Shaffih Dauda, Manara amesema kuwa mtangazaji huyo kuna kipindi aliomba kazi Wasafi TV na alichomolewa nje.

"Mimi najua uliomba ajira pale @wasafitv na wakakutalia mbona hatujapost umevaa T-shirt ya @diamondplatnumz
Unatutafuta ugomvi wa kusudi na mabosi zako tunaowaheshimu sana ila soon Simba itafanya maamuzi makubwa juu yako na Juu ya radio na TV unayoifanya kazi
Au kwa kuwa washabiki wa Yanga walitaka kukupiga ndio maana huandiki habari zao za wachezaji kudai Mishahara ya wachezaji? Simba haina ujinga wa kupiga Waandishi ila tunazo njia sahihi za kukunyoosha…Mara kadhaa umekuwa unaandika upuuzi against us tunakuvumilia tu,sasa sitakuacha,"amemaliza Manara.

Manara na Shaffih Dauda wamekuwa wakiingia kwenye majibizano mazito mara kwa mara, na hii inasemekana ni kutokana na mtangazaji huyo kipindi cha nyuma alishawahi kuomba nafasi ya usemaji wa klabu hiyo.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...