Baada ya tetesi kuwa kiungo mshambuliaji wa klabu ya Simba, Haruna Niyonzima yupo mbioni kujiunga na matajiri Azam FC, Hatimaye tetesi hizo zimeibua vita ya maneno kati ya Msemaji wa Simba, Haji Manara na Mchambuzi wa Soka wa kituo cha redio cha Clouds FM, Shaffih Dauda.
Shaffih Dauda kupitia ukurasa wake wa Instagram aliposti picha ya Niyonzima akiwa amevaa jezi moja iliyowekwa rangi ya Simba na Azam FC na kisha kuiandikia maneno yaliyosomeka "Kwani kuna habari gani?"
Baada ya hapo, Haji Manara aliona sio kesi akaamua kumjibu Shaffih kwa kuandika ujumbe mzito huku akimshambulia mchambuzi huyo kuwa anatumika na ni adui mkubwa wa Simba.
"Tunajua Shaffih unatumika na Maadui wa Simba kutaka kutuvuruga kusudi ili kubalance na cc tuonekane tuna mgogoro na wachezaji wetu!!. Hatuna Niyonzima yupo camp now na leo atacheza ikimpendeza kocha dhidhi ya Bata Bullets, Hivi mtu muungwana kabisa unawezaje kuandika uongo na kufikia kumvalisha jezi ya team nyingine mchezaji aliye na mkataba na klabu yetu kama c uchochezi na uhuni wa kishamba?,"ameandika Haji Manara.
Akiendelea kutupa madogo kwa Shaffih Dauda, Manara amesema kuwa mtangazaji huyo kuna kipindi aliomba kazi Wasafi TV na alichomolewa nje.
"Mimi najua uliomba ajira pale @wasafitv na wakakutalia mbona hatujapost umevaa T-shirt ya @diamondplatnumz
Unatutafuta ugomvi wa kusudi na mabosi zako tunaowaheshimu sana ila soon Simba itafanya maamuzi makubwa juu yako na Juu ya radio na TV unayoifanya kazi
Au kwa kuwa washabiki wa Yanga walitaka kukupiga ndio maana huandiki habari zao za wachezaji kudai Mishahara ya wachezaji? Simba haina ujinga wa kupiga Waandishi ila tunazo njia sahihi za kukunyoosha…Mara kadhaa umekuwa unaandika upuuzi against us tunakuvumilia tu,sasa sitakuacha,"amemaliza Manara.
Manara na Shaffih Dauda wamekuwa wakiingia kwenye majibizano mazito mara kwa mara, na hii inasemekana ni kutokana na mtangazaji huyo kipindi cha nyuma alishawahi kuomba nafasi ya usemaji wa klabu hiyo.
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Kupitia ukurasa wake wa Instagram mjasiriamali Faiza Ally ameweka wazi hisia zake na kusema kuwa anatamani sana kuona msanii wa Bongo Flev...
-
UNAPOTAJA jina la mwanamuziki mkubwa barani Afrika, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' kutoka Tanzania, akili za wengi zinakimbilia kwe...
-
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya siku tano ya kunyesha mvua kubwa inayoweza kusababisha athari ikiwemo mafuriko. ...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Geneva, Switzerland /AFP /.More than 100 groups urged the International Labour Organization to stop taking money from tobacco companies as t...