Muigizaji wa filamu bongo, Yusuph Mlela amefunguka na kudai uwepo wa 'bifu' baina ya Gabo na Duma umewapa faida kubwa kwenye tasnia yao, kwa kuwa bongo movie ilikuwa imepwaya lakini kwa sasa imeanza kuchangamka kutokana na hilo.
Mlela amebainisha hayo alipokuwa anazungumza kwenye kipindi cha FRIDAY NIGHT LIVE 'FNL' kinachorushwa na tinga namba moja kwa vijana EATV, na kusema kwamba ugomvi ni njia pekee inayoweza kuchangamsha soko la filamu kwa kuwa unakuwepo ushindani wa kazi kwa namna moja ama nyingine.
"Sio kitu kibaya kuwepo na bifu, unajua 'game' letu lilikuwa limepoa kwa kiasi fulani, hivyo uwepo wa ugomvi wao inachangamsha tasnia pamoja na kukuza. Tunapenda kuona hivyo angalau bongo movie inakuwa inazungumziwa", amesema Mlela.
Pamoja na hayo, Mlela ameendelea kwa kusema kuwa "nawashauri wasiifanye kiubaya ila waifanye kwa faida ili iwaletee mafanikio na iwe kama mbele wenzetu wanavyofanyaga".
Ugomvi baina ya Gabo Zigamba na Duma ambao wote ni wasanii wa bongo movie ulianza tokea mwaka 2016, mara baada ya Gabo kushinda tuzo ya 'EATV AWARDS' katika kipengele cha muigizaji bora wa kiume ambao waliokuwa wakishindanishwa zaidi ya wasanii wanne akiwepo na Duma katika watu hao, na kupelekea kuanza kutoa maneno yenye kashfa katika siku za mbele yake kuwa hautendei haki ustaa wake kwa madai hajui kuvaa wala kuishi kistaa.
Source
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
