Muigizaji wa filamu bongo, Yusuph Mlela amefunguka na kudai uwepo wa 'bifu' baina ya Gabo na Duma umewapa faida kubwa kwenye tasnia yao, kwa kuwa bongo movie ilikuwa imepwaya lakini kwa sasa imeanza kuchangamka kutokana na hilo.
Mlela amebainisha hayo alipokuwa anazungumza kwenye kipindi cha FRIDAY NIGHT LIVE 'FNL' kinachorushwa na tinga namba moja kwa vijana EATV, na kusema kwamba ugomvi ni njia pekee inayoweza kuchangamsha soko la filamu kwa kuwa unakuwepo ushindani wa kazi kwa namna moja ama nyingine.
"Sio kitu kibaya kuwepo na bifu, unajua 'game' letu lilikuwa limepoa kwa kiasi fulani, hivyo uwepo wa ugomvi wao inachangamsha tasnia pamoja na kukuza. Tunapenda kuona hivyo angalau bongo movie inakuwa inazungumziwa", amesema Mlela.
Pamoja na hayo, Mlela ameendelea kwa kusema kuwa "nawashauri wasiifanye kiubaya ila waifanye kwa faida ili iwaletee mafanikio na iwe kama mbele wenzetu wanavyofanyaga".
Ugomvi baina ya Gabo Zigamba na Duma ambao wote ni wasanii wa bongo movie ulianza tokea mwaka 2016, mara baada ya Gabo kushinda tuzo ya 'EATV AWARDS' katika kipengele cha muigizaji bora wa kiume ambao waliokuwa wakishindanishwa zaidi ya wasanii wanne akiwepo na Duma katika watu hao, na kupelekea kuanza kutoa maneno yenye kashfa katika siku za mbele yake kuwa hautendei haki ustaa wake kwa madai hajui kuvaa wala kuishi kistaa.
Source
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
