Muigizaji wa filamu bongo, Yusuph Mlela amefunguka na kudai uwepo wa 'bifu' baina ya Gabo na Duma umewapa faida kubwa kwenye tasnia yao, kwa kuwa bongo movie ilikuwa imepwaya lakini kwa sasa imeanza kuchangamka kutokana na hilo.
Mlela amebainisha hayo alipokuwa anazungumza kwenye kipindi cha FRIDAY NIGHT LIVE 'FNL' kinachorushwa na tinga namba moja kwa vijana EATV, na kusema kwamba ugomvi ni njia pekee inayoweza kuchangamsha soko la filamu kwa kuwa unakuwepo ushindani wa kazi kwa namna moja ama nyingine.
"Sio kitu kibaya kuwepo na bifu, unajua 'game' letu lilikuwa limepoa kwa kiasi fulani, hivyo uwepo wa ugomvi wao inachangamsha tasnia pamoja na kukuza. Tunapenda kuona hivyo angalau bongo movie inakuwa inazungumziwa", amesema Mlela.
Pamoja na hayo, Mlela ameendelea kwa kusema kuwa "nawashauri wasiifanye kiubaya ila waifanye kwa faida ili iwaletee mafanikio na iwe kama mbele wenzetu wanavyofanyaga".
Ugomvi baina ya Gabo Zigamba na Duma ambao wote ni wasanii wa bongo movie ulianza tokea mwaka 2016, mara baada ya Gabo kushinda tuzo ya 'EATV AWARDS' katika kipengele cha muigizaji bora wa kiume ambao waliokuwa wakishindanishwa zaidi ya wasanii wanne akiwepo na Duma katika watu hao, na kupelekea kuanza kutoa maneno yenye kashfa katika siku za mbele yake kuwa hautendei haki ustaa wake kwa madai hajui kuvaa wala kuishi kistaa.
Source
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Kupitia ukurasa wake wa Instagram mjasiriamali Faiza Ally ameweka wazi hisia zake na kusema kuwa anatamani sana kuona msanii wa Bongo Flev...
-
UNAPOTAJA jina la mwanamuziki mkubwa barani Afrika, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' kutoka Tanzania, akili za wengi zinakimbilia kwe...
-
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya siku tano ya kunyesha mvua kubwa inayoweza kusababisha athari ikiwemo mafuriko. ...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Geneva, Switzerland /AFP /.More than 100 groups urged the International Labour Organization to stop taking money from tobacco companies as t...