Thursday, August 16, 2018
Polisi wayanasa watu 8 kwa kuiba vyuma vya nguzo za umeme
Watu wanane wanaotuhumiwa kuhujumu uchumi Mkoani Morogoro wametiwa mbaroni na jeshi la Polisi kwa tuhuma za kufungua na kuiba vyuma vya nguzo za shirika la umeme nchini Tanesco.
Hayo yamebainishwa na kamanda wa Polisi Mkoani humo, Wilbroad Mutafungwa alipozungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa wananchi wasiokuwa waaminifu wamediliki kukata vyuma vya shirika la umeme na kwenda kuuza kwa matumizi mbalimbali.
Kamanda Mutafungwa amebainisha matumizi ya vifaa hivyo kuwa ni pamoja na kutengenezea majembe ya kulimia ya mkono, milango pia kutengezea baadhi ya sehemu mbalimbali za mitambo.
Aidha ameongeza kuwa vifaa hivyo vinaigharimu Serikali pesa nyingi, hivyo kama jeshi la Polisi lenye mamlaka ya kulinda mali za umma litaendelea na misako mbalimbali ili kuwabaini wahalifu walioko maeneo tofauti tofauti.
"Operesheni hii ni endelevu itaendelea katika Mkoa wote wa Morogoro, hivyo nitoe rai kwa wananchi kama kuna mwenye vyuma kama hivi pengine ulivipata bila kujua tafadhari toa taarifa, lakini itakapokuwa umefikiwa na kikosi kazi kikiongozwa na watu wa shirika la umeme na jeshi la Polisi tukikukamata hautakuwa na nafasi tena ya kujitetea" aliongeza kamanda Mutafungwa.
Pia amewataka wananchi wa maeneo hayo kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo pindi wanapowabaini watu wenye nia ovu ya kuhumu uchumi nchi, hivyo rai yeyote mwenye vifaa hivyo avisalimisha ili kuendelea kuijenga nchi.
Kwa upande wake Afisa usalama wa Tanesco mkoani Morogoro Charles Ngwila amesema katika opesheni hiyo walioshirikiana na jeshi la polisi wamefanikiwa kuwakamata watu wanane na vyuma 117 katika maeneo ya Mang'ula na Pelege wilayani Kilombero.
Hivyo amewasihi wananchi wote wenye taarifa ya wahalifu watoe taarifa Tanesco na polisi ili wote wanaohusika na vitendo hivyo waweze kuchukuliwa hatua za kisheria.
Watuhumiwa hao nane walikamatwa Wilayani Ifakara wamefikishwa mahakamani kwenda kujibu mashtaka yanayowakabili ikiwa pamoja na uhujumu uchumi.
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Wanajeshi wawili wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa wamejeruhiwa baada ya kifaru cha Israel kufyatua risasi kuelekea mnara wa Umoja wa M...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Mamlaka za China zipo mbioni kudhibiti ongezeko la harusi za kifahari amabazo zimekuwa zikishamiri katika miaka ya karibuni. Kwamujibu wa ma...
-
Kupitia ukurasa wake wa Instagram mjasiriamali Faiza Ally ameweka wazi hisia zake na kusema kuwa anatamani sana kuona msanii wa Bongo Flev...
-
Katika kila makabiliano ya kijeshi kati ya Israel na Lebanon, bila kujali ni upande gani unaopigana huko Lebanon, Mto Litani, moja ya mito...