Thursday, August 16, 2018
Polisi wayanasa watu 8 kwa kuiba vyuma vya nguzo za umeme
Watu wanane wanaotuhumiwa kuhujumu uchumi Mkoani Morogoro wametiwa mbaroni na jeshi la Polisi kwa tuhuma za kufungua na kuiba vyuma vya nguzo za shirika la umeme nchini Tanesco.
Hayo yamebainishwa na kamanda wa Polisi Mkoani humo, Wilbroad Mutafungwa alipozungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa wananchi wasiokuwa waaminifu wamediliki kukata vyuma vya shirika la umeme na kwenda kuuza kwa matumizi mbalimbali.
Kamanda Mutafungwa amebainisha matumizi ya vifaa hivyo kuwa ni pamoja na kutengenezea majembe ya kulimia ya mkono, milango pia kutengezea baadhi ya sehemu mbalimbali za mitambo.
Aidha ameongeza kuwa vifaa hivyo vinaigharimu Serikali pesa nyingi, hivyo kama jeshi la Polisi lenye mamlaka ya kulinda mali za umma litaendelea na misako mbalimbali ili kuwabaini wahalifu walioko maeneo tofauti tofauti.
"Operesheni hii ni endelevu itaendelea katika Mkoa wote wa Morogoro, hivyo nitoe rai kwa wananchi kama kuna mwenye vyuma kama hivi pengine ulivipata bila kujua tafadhari toa taarifa, lakini itakapokuwa umefikiwa na kikosi kazi kikiongozwa na watu wa shirika la umeme na jeshi la Polisi tukikukamata hautakuwa na nafasi tena ya kujitetea" aliongeza kamanda Mutafungwa.
Pia amewataka wananchi wa maeneo hayo kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo pindi wanapowabaini watu wenye nia ovu ya kuhumu uchumi nchi, hivyo rai yeyote mwenye vifaa hivyo avisalimisha ili kuendelea kuijenga nchi.
Kwa upande wake Afisa usalama wa Tanesco mkoani Morogoro Charles Ngwila amesema katika opesheni hiyo walioshirikiana na jeshi la polisi wamefanikiwa kuwakamata watu wanane na vyuma 117 katika maeneo ya Mang'ula na Pelege wilayani Kilombero.
Hivyo amewasihi wananchi wote wenye taarifa ya wahalifu watoe taarifa Tanesco na polisi ili wote wanaohusika na vitendo hivyo waweze kuchukuliwa hatua za kisheria.
Watuhumiwa hao nane walikamatwa Wilayani Ifakara wamefikishwa mahakamani kwenda kujibu mashtaka yanayowakabili ikiwa pamoja na uhujumu uchumi.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
