Msanii wa filamu bongo, Daudi Michael maarufu kama 'Duma' amedai wasanii wengi wameshindwa kuendelea kuishi katika soko la filamu nchini kutokana na kuzoea kupewa fedha na baadhi ya wasambaji ili kusudi waweze kufanya kazi waliotumwa jambo ambalo kwa sasa watu hao hawafanyi tena.
Duma amebainisha hayo wakati alipokuwa anazungumza na www.eatv.tv baada ya kuwepo wimbi kubwa la wasanii kupungua katika soko la filamu, jambo ambalo wafuatiliaji na wapenzi wa tasnia hiyo kudai huenda bongo movie imekufa au kutolipa katika nyakati hizi.
"Ninapambana na nitaendelea kufanya hivyo hadi tone langu la mwisho, ili kusudi soko la filamu liweze kurudi kwenye 'chart' yake kama ilivyokuwa hapo awali. Sitoweza kukubali kushindwa katika hili", amesema Duma.
Mbali na hilo, Duma amefafanua baadhi ya mambo kuwa kinachowafanya wasanii wengi wa filamu kushindwa kutoa kazi zao kama ilivyokuwa hapo awali ni kutokana na ma-boss waliokuwa wanawapa fedha, sasa hawatoi tena.
"Ma-boss hawatoi fedha tena sasa hivi kutokana kutosheka na movie walizokuwa nazo, wasanii waliowengi hawamiliki filamu za kwao binafsi bali wao wanakuwa kama vibarua tu wa kufanyakazi kutokana na bajeti walizopewa na watu hao", amesisitiza Duma.
Kwa upande mwingine, Duma anatarajia kuachia kazi yake mpya kesho inayokwenda kwa jina la 'nipe changu', ambayo imejumuisha wasanii mbalimbali pamoja na kuwa na maudhui ya kitofauti na jinsi watanzania walivyozoea kuzitazama.
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Wanajeshi wawili wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa wamejeruhiwa baada ya kifaru cha Israel kufyatua risasi kuelekea mnara wa Umoja wa M...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Mamlaka za China zipo mbioni kudhibiti ongezeko la harusi za kifahari amabazo zimekuwa zikishamiri katika miaka ya karibuni. Kwamujibu wa ma...
-
Kupitia ukurasa wake wa Instagram mjasiriamali Faiza Ally ameweka wazi hisia zake na kusema kuwa anatamani sana kuona msanii wa Bongo Flev...
-
Katika kila makabiliano ya kijeshi kati ya Israel na Lebanon, bila kujali ni upande gani unaopigana huko Lebanon, Mto Litani, moja ya mito...