Msanii wa filamu bongo, Daudi Michael maarufu kama 'Duma' amedai wasanii wengi wameshindwa kuendelea kuishi katika soko la filamu nchini kutokana na kuzoea kupewa fedha na baadhi ya wasambaji ili kusudi waweze kufanya kazi waliotumwa jambo ambalo kwa sasa watu hao hawafanyi tena.
Duma amebainisha hayo wakati alipokuwa anazungumza na www.eatv.tv baada ya kuwepo wimbi kubwa la wasanii kupungua katika soko la filamu, jambo ambalo wafuatiliaji na wapenzi wa tasnia hiyo kudai huenda bongo movie imekufa au kutolipa katika nyakati hizi.
"Ninapambana na nitaendelea kufanya hivyo hadi tone langu la mwisho, ili kusudi soko la filamu liweze kurudi kwenye 'chart' yake kama ilivyokuwa hapo awali. Sitoweza kukubali kushindwa katika hili", amesema Duma.
Mbali na hilo, Duma amefafanua baadhi ya mambo kuwa kinachowafanya wasanii wengi wa filamu kushindwa kutoa kazi zao kama ilivyokuwa hapo awali ni kutokana na ma-boss waliokuwa wanawapa fedha, sasa hawatoi tena.
"Ma-boss hawatoi fedha tena sasa hivi kutokana kutosheka na movie walizokuwa nazo, wasanii waliowengi hawamiliki filamu za kwao binafsi bali wao wanakuwa kama vibarua tu wa kufanyakazi kutokana na bajeti walizopewa na watu hao", amesisitiza Duma.
Kwa upande mwingine, Duma anatarajia kuachia kazi yake mpya kesho inayokwenda kwa jina la 'nipe changu', ambayo imejumuisha wasanii mbalimbali pamoja na kuwa na maudhui ya kitofauti na jinsi watanzania walivyozoea kuzitazama.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
