Mwenyekiti wa TLP, Augustino Mrema amemtaka waziri wa mambo ndani, Kangi Lugola kuwachukulia hatua wabunge wanaomchafua Rais John Magufuli.
Amesema kuna vikundi vya wabunge ambao wanatengeneza chokochoko dhidi ya Rais na kwamba hatua zichukuliwe kabla hawajatimiza azma yao mbaya dhidi yake.
Akizungumza na waandishi wa habari jana Agosti 3 katika ofisi za chama hicho zilizopo Magomeni, Dar es Salaam, Mrema amesema wabunge hao ambao baadhi ni wanachama wa CCM wanahatarisha usalama wa Rais kwa kumchonganisha na wananchi.
Mrema ambaye alikuwa Waziri wa Mambo ya Ndani katika serikali ya awamu ya pili amesema anawafahamu wabunge hao licha ya kutowataja majina yao.
Ameahidi kumpa ushirikiano Waziri Lugola endapo atahitaji kwa kuwa anafahamu mambo hayo kiundani.
"Mimi nimewasikiliza wabunge tena wa CCM kwa mfano waliosema Rais amechukua Trilioni 1.5 ni kweli au ni kumchafua? Kwa hiyo kuna hiyo tabia imezuka ya kumzulia Rais maneno ya uongo na ya kumdhoofisha,"alisema.
Alisema vikundi hivyo nimekuwa vikitengeneza "chokochoko" ambazo zinalenga kumchonganisha Rais na wananchi.
"Wabunge hao nawafahamu na niko tayari kuwataja kabla hawajatimiza uovu kama ilivyokuwa kwangu,"amesema.
Alieleza kuwa atakuwa mstari wa mbele kuhakikisha Rais anaheshimiwa na kuungwa mkono kwa sababu kazi aliyonayo ni kubwa.
Pia amemshauri Rais Magufuli kuwa makini na viongozi wake kwa kuwa wengi wanafanya mambo kwa kutafuta 'kiki' na huenda wakawa si rafiki katika kazi zake.
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Kupitia ukurasa wake wa Instagram mjasiriamali Faiza Ally ameweka wazi hisia zake na kusema kuwa anatamani sana kuona msanii wa Bongo Flev...
-
UNAPOTAJA jina la mwanamuziki mkubwa barani Afrika, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' kutoka Tanzania, akili za wengi zinakimbilia kwe...
-
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya siku tano ya kunyesha mvua kubwa inayoweza kusababisha athari ikiwemo mafuriko. ...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...