Tuesday, March 4, 2025
Rais Samia apongezwa kwa kutoa sadaka ya iftari kwa wahitaji Tanga
Mufti Mkuu wa Tanzania Shekh Abubakary Zuberi Bin Ally amewataka waumini wote wa dini ya kiislam nchini kuitunza neema waliopewa na Mungu hususani kipindi huki cha Mfungo wa Ramadhani .
Hayo aliyasema wakati akizungumza katika msikiti wa Tamta uliopo jijini Tanga ambapo walifuturisha watu mbalimbali wakiwemo watoto yatima na wenye uhitaji kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samaia Suluhu Hassan.
Aidha alisema kuwa ni vyemq waumuini kuitunza neema waliojaaliwa na Mungu kwani neema ya Mungu ndio inayowalinda katika maisha yao, sambamba hayo alimshukuru Rais Samia kwa kuwashirikisha viongozi wa dini katika ziara yake ya siku saba katika mkoa wa Tanga.
Kwa Upande wake Mwenyeiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajabu Abdulrahaman Abdalah alisema wanamshukuru na kumpongeza Rais Samaia Siluhu Hassan kwa kuvunja rekodi ya kukaa kwa siku siku saba katika mkoa wa Tanga kwani haijawahi kutokea.
Naye Mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian amewaponeza na kuwashukuru wananchi wa Mkoa wa Tanga kwa mapokezi mazuri ya Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samaia Siluhu Hassan Tangu alipoanza ziara Yake ya Kikazi mkoani humo ambapo alitembelea wilaya zote ndani ya mkoa.
Alisema kwa namna ambayo wananchi waliitokeza kwa wengi serikali imefarijika sana na tunawaahidi kuendelea kushikamana siku zote kwani wameishimisa serikali mkoa jambo ambalo limedhihirisha Upendo kwa Mh.Rais Dkt Samia.
Balozi Buriani alisema kuwa ujio wa Rais Dkt. Samia kwa mkoa Tanga umeleta hamasa kubwa kwani amezindua miradi mingi iliyogharimu kiasi cha sh.Tirilion moja na Milioni Mia nane jambo ambalo imeonyesha kuwa kazi kubwa iliyofanywa na serikali .
"Tumshukuru sana rais kwa kutuzinduliwa miradi mikubwa ikiwemo Bandari uliogharimu Bilion 429 ,jengo la utawala Bumbuli wilayani Lushoto,Hospitali ya wilaya ya Handeni ,Mradi wa maji wa miji 28 na miradi mingine mingi ." alisema Balozi Buriani
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
