Thursday, July 22, 2021

Tanzia: ALIYEKUWA MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO ANNA MGHWIRA AFARIKI DUNIA




Aliyewahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Elisha Mghwira


Aliyewahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, na mgombea Urais nchini Tanzania kupitia Chama cha ACT-Wazalendo katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, Anna Elisha Mghwira, amefariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Mount Meru, Arusha.

Imeelezwa kuwa Mama Mghwira amefariki dunia leo Julai 22, 2021, majira ya mchana, ambapo taarifa zinadai kwamba wiki moja iliyopita alikuwa amelazwa katika Hospitali ya Nkoaranga kwa tatizo la kupumua ambapo baadaye hali yake kuwa mbaya alihamishiwa hospitali ya Mount Meru

Chanzo- EATV

Source
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...