Wednesday, July 7, 2021

Mazungumzo kuhusu Afghanistan yaanza rasmi Iran


Mazungumzo juu ya Afghanistan yameanza nchini Iran.


Wawakilishi wa serikali ya Afghanistan na Taliban wamekwenda mji mkuu wa Iran, Tehran, kufanya mazungumzo yaliyoandaliwa na Iran.


Kulingana na taarifa iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya nje ya Iran, mazungumzo kati ya serikali ya Afghanistan na Taliban yalianza na hotuba ya Waziri wa Mambo ya nje Mohammad Javad Zarif.


"Watu wa Afghanistan na viongozi wao wa kisiasa lazima wafanye maamuzi mazito leo kwa mustakabali wa nchi yao." alisema.


Akielezea kuwa kurudi kwenye meza ya mazungumzo na njia za kisiasa ni chaguo bora, Zarif amesema kuwa wako tayari kusaidia mgogoro kati ya Waafghanistan.


Imeelezwa kuwa ujumbe wa serikali ya Afghanistan uliongozwa na Waziri wa zamani wa Mambo ya nje Yunus Suleiman na ujumbe wa Taliban uliongozwa na Abbas Istankizi, naibu mkuu wa ofisi ya kisiasa ya shirika hilo.


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...