Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amesema kuwa, utekelezaji wa mradi mkubwa wa kufua umeme kwa maji wa Julius Nyerere kwenye maeneo muhimu umefikia asilimia 51.5 kwa sasa.
Dkt. Kalemani ameyasema hayo Mei 22, 2021 alipokuwa kwenye ziara ya kukagua hatua za utekelezaji mradi huo wa Julius Nyerere akiambatana na Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi kutoka Misri, Dkt. Assem Elgazzar.
Dkt. Kalemani ameyataja maeneo ya ujenzi huo yaliyokamilika kwa asilimia hizo kwa ujumla wake kuwa ni, ujenzi wa tuta kuu, ujenzi wa wa jumba la kuendeshea mitambo, ujenzi wa njia za kupeleka maji kwenye mitambo ya kufua umeme pamoja na kituo cha kupokea na kusafirisha umeme wa msongo wa kilovolti 400.
"Mbali ya utekelezaji wa mradi kufika hatua hiyo lakini pia hadi sasa Mkandarasi ameshalipwa shilingi trilioni 2.4 kulingana na mpango kazi" amesema Dkt. Kalemani.
Katika hatua nyingine transfoma sita kati ya ishirini na saba zitakazofungwa kwenye kituo cha kupokea umeme zimewasili, ambapo Dkt. Kalemani ameiagiza ziharakishwe kutolewa Bandarini na kupelekwa eneo la mradi ili kazi ya kuzifunga ianze.
Kwa upande wake Waziri wa Nyumba na Makazi kutoka Misri Dkt. Assem Elgazzar amesema kuwa, Serikali ya Misri inaendelea kuusimamia mradi na kuahidi utakamilika kwa wakati mwezi Juni 2022 kama ilivyo kwenye mkataba.
Awali akielezea maendeleo ya utekelezaji wa mradi kwa niaba ya Mhandisi Mkazi, Mhandisi Lutengano Mwandambo kutoka TECU amesema timu ya wataalamu kutoka Tanzania imeenda kukagua utengenezaji wa mitambo ya kufua umeme itakayotumika katika mradi huo.
Aliongeza kuwa, kufikia mwezi Novemba mwaka huu kazi ya kujaza maji kwenye bwawa itaanza ambapo itakwenda hadi Aprili mwaka 2022 ambapo kiwango cha maji kitakuwa kimefikia kina cha 163 juu ya usawa wa bahari, kiwango ambacho kinatosha kuanza kufua umeme.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
