Monday, February 8, 2021
Taarifa Ya Utekelezaji Maamuzi Ya Serikali Kuhusu Migogoro Ya Matumizi Ya Ardhi Katika Vijiji 975 Yawasilishwa
Na Munir Shemweta, WANMM DODOMA
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvu amewaoongoza Mawaziri wenzake wa Wizara za Kisekta kupokea taarifa ya utekelezaji wa maamuzi ya Serikali kuhusu Migogoro ya matumizi ya ardhi katika vijiji 975 vilivyopo katika hifadhi na Mapori ya Akiba.
Taarifa hiyo iliwasilishwa na Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mary Makondo tarehe 4 Februari 2021 jijini Dodoma kwa niaba ya Kamati ya Mawaziri na Wataalamu kutoka Wizara za Kisekta.
Wizara za kisekta zinazoshiriki ni Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Maliasili na Utalii, Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Ofisi ya Makamu wa Raisi, Wizara ya Ulinzi na Wizara ya Maji. Aidha, katika kikao hicho Wizara za Mambo ya Ndani Nchi, Wizara ya Katiba na Sheria na Wizara ya Fedha zilialikwa kutokana na umuhimu wa wizara hizo katika utekelezaji wa maamuzi.
Akizungumza wakati wa uwasilishwaji taarifa hiyo, Waziri wa Ardhi William Lukuvi alisema, mbali na mambo mengine Taarifa ya vijiji 975 vyenye migogoro ya matumizi ya ardhi itawezesha Mawaziri wa Wizara husika aliowaeleza kuwa, wengi wao ni wageni kujua mpango mkakati na namna ya utekelezaji wa maamuzi ya Serikali kuhusiana na kunusuru vijiji 975.
''Hapa wengi wenu ni wageni karibu asilimia 80, hivyo taarifa inayowasilishwa leo itawasaidia kujua utekelezaji wa maamuzi ya serikali kuhusiana na migogoro ya matumizi ya ardhi katika vijiji 975'' alisema Lukuvi.
Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mary Makondo alisema kupitia kikao hicho kuwa, pamoja na Kamati kutekeleza maamuzi ya Serikali kuhusiana na migogoro ya matumizi ya ardhi kwenye vijiji 975, wizara yake imetekeleza pia baadhi ya mambo kwa lengo la kupunguza migogoro ya matumizi ya ardhi kama vile kuandaa mpango wa matumizi ya ardhi katika vijiji 114 vinavyozunguka hifadhi.
Utekelezaji wa maamuzi ya Serikali kuhusiana na migogoro ya matumizi ya ardhi katika vijiji 975 nchini unafuatia kukithiri kwa migogoro ya ardhi ambapo, Dkt. John Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Februari 2019 aliunda Kamati ya Mawaziri wa Kisekta chini ya Waziri wa Ardhi William Lukuvi ili kutafuta ufumbuzi wa kudumu.
Kufuatia mapendekezo ya Kamati, Baraza la Mawaziri mnamo mwezi Septemba, 2019, liliridhia kuwa vijiji 920 kati ya vijiji 975 vilivyokuwemo ndani ya hifadhi na mapori visiondolewe.
Source
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
