Thursday, February 11, 2021

Air Namibia yasitisha safari zake



Namibia imeamua kusitisha safari zote za ndege ya taifa ya Air Namibia.

Kampuni hiyo ya ndege imewataka wateja wote kuomba kurejeshewa fedha zao na kusitisha safari zao.

Tangazo hilo limesababisha ajira za watu zaidi ya 600 kupotea , gazeti la taifa hio limeripoti.

Maamuzi hayo yametoka kwa baraza la mawaziri la kutaka safari zisitishwe, taarifa ya gazeti hilo imeeleza.

Wafanyakazi watapokea mshahara kwa kipindi cha miezi 12 ijayo ila hawatapata mafao, Shirika la habari la Namibia limeripoti.

Ndege hiyo ilikuwa na misukosuko ya uendeshaji wake -wiki iliyopita wajumbe wa bodi walijiuzuru wakiishutumu serikali kuingilia kati masuala ya ndege hiyo.

Kwa mujibu wa tovuti ya Aviation24.be - tovuti inayotoa taarifa kuhusu masuala ya anga-imesema Namibia Air ilikuwa na changamoto za kifedha na suala la tatizo la usalama, na kuibuka kwa janga la corona ndio kumeifanya sekta ya usafirishaji kuanguka kabisa.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...