Kama wewe ni mtu unayependa kujifunza kutenegeneza vitu vya kijasiriamali basi makala hii ni maalumu sana kwako.
Mahitaji:
1. Vibanio vyenye urembo mbalimbali.
2. Sponji zenye urembo mbalimbali.
3. Brash kubwa/ndogo.
4. Meza kubwa yenye urefu wa mita moja mpaka mbili.
5. Sufuria.
6. Vitambaa vya mpira.
7. Misumari midogo.
8. Jiko.
Madawa:
1. Sodium hydrosulphate.
2. Caustic soda
3. Mshumaa.
Kazi zake:
1. Sodium hydrosulphate ni kuimarisha rangi isichuje, kama itachanganywa na caustic soda. Madawa haya huwa kazi yake ni moja lakini ikikosekana moja nyingine haifanyi kazi.
2. Kazi ya mshumaa ni kuweka urembo kwenye nguo au kwenye vitambaa kwa kutumia vibao au sponji zenye urembo wa tembo, twiga, matunda au aina yoyote ya urembo unayotaka mtengenezaji.
Jinsi ya kutengeneza.
Jinsi ya kugonga mishumaa
Chemsha mshumaa uchemke sawasawa kisha ipua upoekidogo.Andaa kitambaa cha cotton na kukitandika mezani,chovya kibao chenye picha kwenye mshumaa kisha gonga kwenye kitambaa na kuacha nafasi kidogo. Endelea kugonga picha hizo mpaka kitambaa kiishe.
Jinsi ya kuweka rangi
Chemsha maji ya moto yachemke sawa sawa kisha pima lita tano mpaka sita. Baada ya hapo pima caustic soda vijiko3 na sodium hydrosulphate vijiko vinne mpaka vitano. Changanya na maji ya moto ,weka rangi kijiko kimoja. Baada ya hapo pima maji lita kumi na tano na changanya na mchanganyiko wa madawa ili maji yawe vuguvugu.Tumbukiza vitambaa vya vinne vya mita tatu kwa wakati mmoja na kuvigeuzageuza viingie rangi kwa dakika kumi mpaka kumi na tano. Suuza kwa maji baridi na uanike kwenye kivuri ili mshumaa usiyeyuke.
Kuweka rangi ya pili
Katika kuweka rangi hii kinachofanyika ni kuongeza vipimo vya ranagi tu. Ongeza vipimo vya rangi viwili na zaidi ya mala ya kwanza, maji, mudani uleule.
Weka mshumaa sehemu ambayo haina mshumaa kwa kutumia urembo uleule. Pima rangi kwa kufuata hatua zilezile. Tumbukiza vitambaa vitatu, geuza kwa mda uleule kisha anika.
Jinsi ya ufua mshumaa
Chemsha maji yachemke vizuri, changanya na sabuni ya unga jikoni, tumbukiza kitambaa kimoja kimoja jikoni ili kutoa mshumaa, geuza kwa mti, suuza kwenye maji ya baridi yaliyochanganywa na maji.
Piga pasi tayari kwa kuuza.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
