Saturday, November 14, 2020
Watalii Wa Ndani Zaidi Ya 80 Watembelea Hifadhi Ya Ngorongoro
Na Kassim Nyaki-NCAA
Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) imepokea zaidi ya watalii wa ndani 80 kutoka benki ya CRDB kwa ajili ya kutembelea vivutio mbalimbali vinavyopatikana katika hifadhi hiyo ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha utalii wa ndani (domestic tourism).
Safari ya watalii hao iliyoratibiwa na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) kwa kushirikiana Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro imelenga kutoa hamasa kwa watanzania kutembelea vivutio mbalimbali vinavyopatikana nchini ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono jitihada za Serikali kutangaza vivutio hivyo ambavyo vimekuwa na mchango mkubwa katika kuongeza pato la Taifa.
Mkurugenzzi wa Masoko wa TTB Mindi Kasiga aliyeambatana na ujumbe huo amebainisha kuwa, ujio wa wageni hao ni muendelezo wa juhudi za Serikali kuhamasisha watanzania na wageni wa mataifa mbalimbali kutembelea vivutio vya utalii vilivyoko nchini ili kutoa hamasa kwa wananchi.
"Nchi yetu imebarikiwa kuwa na vivutio vingi na vya kipekee duniani, TTB kwa kushirikiana na NCAA tumeandaa programu hii ikiwa ni muendelezo wa kuunga mkono juhudi za Serikali kutangaza vivutio vyetu ndani na nje ya nchi na tunafurahi kuona kwamba muoamko wa Watanzania kutembelea vivutio vyetu umezidi kuimarika kila mwaka"), aliongeza Kasiga.
Kwa upande wake Kamishna msaidizi mwandamizi wa UhIfadhi (huduma za Utalii) wa NCAA Bw. Paul Fissoo ameipongeza TTB na CRDB kwa kuleta kundi la wafanyakazi zaidi ya 80 kutembelea hifadhi hiyo kwa wakatii mmoja na kusisitiza kuwa utaratibu huo ni mfano mzuri wa kuigwa kwa mashirika mengine ya Serikali na Sekta binafsi kuandaa safari za pamoja na watumishi wao ili kutembelea vivutio vya hifadhi hiyo kwa bei nafuu kabisa ya shilingi 11,800 pekee.
Eneo la Hifadhi ya ngorongro ni eneo lenye vivutio vya kipekee duniani ikiwemo Crater ya Ngorongoro yenye Wanyama wa aina mbalimbali zaidi ya 25000, utalii wa kiutamaduni, makumbusho yenye historia ya chimbuko ya binadamu wa kale zaidi duniani (Zamadam), nyayo za binadamu wa kale, pia ni eneo pekee ambapo unaweza kuwaona Wanyama wakubwa watano (Simba, faru, Chui, Tembo na Nyati) kwa wakati mmoja katika eneo moja.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
