Manuel Merino, ambaye alichukua wadhifa wa rais wa mpito baada ya Rais Martin Vizcarra kufutwa kazi nchini Peru mnamo Novemba 11, amejiuzulu.
Kulingana na habari katika vyombo vya habari vya Peru, Merino ametangaza kwamba amejiuzulu kupitia hotuba yake ya moja kwa moja baada ya Bunge kumtaka ajiuzulu baada ya maandamano ya barabarani ambayo watu 2 walifariki na zaidi ya watu 100 walijeruhiwa.
Moreno, ambaye alitishiwa na Congress kuwa atafukuzwa ikiwa hatajiuzulu, alisema kwenye runinga:
"Nataka kujiuzulu kwangu kukubaliwa na watu wa Peru."
Tangu mwanzoni mwa juma, mawaziri 13 kati ya 18 katika baraza la mawaziri wamejiuzulu baada ya maelfu ya wafuasi wa Vizcarra kumtaka Merino aondoke ofisini na watu 2 kufariki katika maandamano huko San Martin Square na Mtaa wa Albancay huko Lima.
Kujiuzulu kwa Merino kumesheherekewa katika mitaa ya Peru.
Source
