Monday, June 8, 2020
Breaking: Lissu atangaza rasmi nia ya kuwania Urais
Mwanansiasa wa upinzani nchini Tazanzania Tundu Lissu hii leo ametangaza rasmi nia ya kuwania urais kupitia chama chake cha Chadema.
Akizungumza kwa njia ya mitandao akiwa ughaibuni, Lissu ametangaza nia ya kuwania urais nchini Tanzania, uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka 2020.
Lissu ametangaza nia hiyo akiwa ughaibuni ambako alipelekwa miaka takribani miaka mitatu iliyopita baada ya kushambuliwa vibaya kwa risasi na watu wasiojulikana.
''Sasa ninapenda kuwataarifu rasmi kwamba nimetangaza rasmi nia yangu ya kugombea nafasi ya urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.Tayari nimeshawasilisha taarifa rasmi ya kutangaza nia hiyo kwa katibu mkuu wa chama chetu kama iliyoelekezwa kwenye maelekezo yake kwa wanachama wa chama chetu.''
Katika hotuba yake iliyopeperushwa mubashara mchana huu kwa njia ya mitandao ya kijamii, Lissu ameahidi kuwa endapo atapata ridhaa ya kuiongoza Tanzania serikali yake haitalipiza kisasi.
Source
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
