Monday, June 8, 2020
Breaking: Lissu atangaza rasmi nia ya kuwania Urais
Mwanansiasa wa upinzani nchini Tazanzania Tundu Lissu hii leo ametangaza rasmi nia ya kuwania urais kupitia chama chake cha Chadema.
Akizungumza kwa njia ya mitandao akiwa ughaibuni, Lissu ametangaza nia ya kuwania urais nchini Tanzania, uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka 2020.
Lissu ametangaza nia hiyo akiwa ughaibuni ambako alipelekwa miaka takribani miaka mitatu iliyopita baada ya kushambuliwa vibaya kwa risasi na watu wasiojulikana.
''Sasa ninapenda kuwataarifu rasmi kwamba nimetangaza rasmi nia yangu ya kugombea nafasi ya urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.Tayari nimeshawasilisha taarifa rasmi ya kutangaza nia hiyo kwa katibu mkuu wa chama chetu kama iliyoelekezwa kwenye maelekezo yake kwa wanachama wa chama chetu.''
Katika hotuba yake iliyopeperushwa mubashara mchana huu kwa njia ya mitandao ya kijamii, Lissu ameahidi kuwa endapo atapata ridhaa ya kuiongoza Tanzania serikali yake haitalipiza kisasi.
Source
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
